UPANDAJI MITI: WAZIRI MKUU AUNGA MKONO MAADHIMISHO YA KIZALENDO YA RAIS SAMIA

 


                              


WAZIRI MKUU

DODOMA

Na Mwandishi wetu

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, ameshiriki katika zoezi la upandaji miti lililofanyika mbele ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma.

Zoezi hilo ni sehemu ya jitihada za kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia uamuzi wake wa kizalendo wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo vinavyolenga kulinda na kuhifadhi mazingira.

Akizungumza baada ya zoezi hilo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu, akiwa ameambatana na mwenza wake Mama Neema Mwigulu, alimpongeza Rais Dkt. Samia kwa uongozi wake thabiti unaoendelea kudhihirisha maono, ubunifu na dhamira ya kulinda maslahi mapana ya Taifa.

Alisema kuwa zoezi hilo limeleta utofauti mkubwa kwa kuchochea upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali nchini, akibainisha kuwa katika vitabu vitukufu, kupanda mti ni miongoni mwa ibada kutokana na manufaa makubwa yanayowafikia watu wengi.

Aidha, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliwahimiza Watanzania kuiga mfano huo kwa kuadhimisha siku zao za kuzaliwa kwa kupanda miti. Alisisitiza kuwa nyakati za kumbukumbu kama hizo zitumike kufanya matendo yenye kuacha alama chanya na manufaa kwa jamii.

Katika zoezi hilo, Mheshimiwa Waziri Mkuu alipanda mti wa aina ya MDODOMA/MTIMAJI (Trichilia emetica).



Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments