MKUU WA MKOA SINGIDA: UJUZI WA UFUNDI STADI NI MSINGI WA MAENDELEO.(PICHA NA MATUKIOYA KILELE CHA VETA )

 







                            


                            
                              Hapa kazi tu kwa Vitendo katika jengo Manispaa ya Singida 



Picha za matukio mbalimbali yaliyojiri katika maadhimisho ya kanda ya Kati ya Veta 

Singida

Na Mwandishi Wetu

Wito umetolewa kwa Vijana wanaomaliza masomo yao katika vyuo vikuu na vya kati wamehimizwa kujiunga na vyuo vya ufundi stadi ili kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kuimarisha maisha yao kiuchumi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, alitoa wito huo alipofunga maadhimisho ya miaka 30 ya VETA na miaka 50 ya utoaji wa elimu ya ufundi stadi Kanda ya Kati. Amesema mkoa umejipanga kuweka mikakati madhubuti ili kuwawezesha vijana kupata ujuzi huo kwa urahisi.

Aidha, Dendego alipongeza vyuo vya VETA kwa mchango wao mkubwa katika kuwaandaa vijana kupitia mafunzo ya vitendo. Akiwa katika ziara, alitembelea ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri ya Manispaa ya Singida, unaotekelezwa na mafundi waliopitia VETA, na kuwasisitiza vijana kujiunga na vyuo hivyo ili kuongeza maarifa yao ya ufundi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati, Ramadhani Makata, alisema serikali imeendelea kuboresha mazingira ya elimu ya ufundi kwa kuhakikisha mafunzo hayo yanapatikana kwa gharama nafuu. Alibainisha kuwa zaidi ya shilingi bilioni 27 zinatumika katika ujenzi wa vyuo 18 vya VETA katika mikoa ya Dodoma, Singida, na Manyara, ambapo vyuo tisa tayari vimekamilika.



Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments