NAIBU WAZIRI KATAMBI: RUSU WAFANYAKAZI KUSHIRIKI MICHEZO – MEI MOSI SINGIDA

Naibu waziri wa ofisi ya Waziri mkuu kazi vijana Ajira na watu wenye ulemavu Mhe, Potrobas Katambi






    
                             
                             Angalia Jabu biingwa wa mashindano ya kivuta kamba taifa .

Singida

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Vijana, Kazi, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi, amezitaka taasisi na wizara zote kuhakikisha kuwa zinatoa ruhusa kwa wafanyakazi wao kushiriki kikamilifu katika michezo ya Mei Mosi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa michezo ya Mei Mosi kitaifa, inayofanyika katika uwanja wa CCM LITI mkoani Singida, Mhe. Katambi amesema michezo si tu burudani bali ni jukwaa muhimu la kuimarisha mahusiano, mshikamano na afya miongoni mwa watumishi wa umma na sekta binafsi.

"Michezo ni njia ya kujenga afya lakini pia ni sehemu ya mahusiano bora kazini. Wafanyakazi wakishiriki michezo wanarudi kazini wakiwa na morali mpya na afya njema," alisema Mhe. Katambi.

Kwa upande wake, Katibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) taifa, Hery Mkunda alieleza kuwa Mei Mosi ya mwaka huu itakuwa ya kipekee, si tu kwa ukubwa wa tukio bali kwa namna maandalizi yalivyofanyika kwa ubunifu na umakini mkubwa chini ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Halima Dendego.

"Mwaka huu Mei Mosi si ya kawaida, Singida imeweka historia kwa namna ilivyopokea jukumu hili na kulitekeleza kwa weledi. Tunawashukuru viongozi wa mkoa kwa ushirikiano wao mkubwa," alisema Katibu huyo wa TUCTA.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mei Mosi Kitaifa, Bw. Michael Masubo, amepongeza mkoa wa Singida kwa kuonesha utayari mkubwa na ushirikiano wa karibu katika maandalizi ya michezo hiyo.

“Singida ni mkoa wa kipekee. Nampongeza Mkuu wa Mkoa, Dkt. Dendego, kwa kushiriki kwa karibu kila hatua ya maandalizi haya na kuhakikisha kila kitu kinaenda kwa wakati,” alisema Masubo.

Katibu Mkuu wa Kamati ya Maandalizi ya Mei Mosi, Bw. Alex Temba, ameongeza kuwa mbali na mashindano ya michezo yanayoendelea, kutakuwa na matukio mbalimbali ya kijamii na burudani kuelekea kilele cha sherehe hiyo tarehe 1 Mei.

Akitangaza ratiba ya michezo hiyo, Bw. Temba alieleza kuwa michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, netiboli, kuvuta kamba, na mbio za watumishi itafanyika kwa siku kadhaa kabla ya kilele cha sherehe hiyo ya wafanyakazi duniani.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments