MBIO ZA MITA 100 KWA WAZEE WA MIAKA 50 ZAVUTIA WENGI

 







Singida

Katika kuelekea maadhimisho ya Mei Mosi mwaka huu, michezo mbalimbali inaendelea kufanyika mkoani Singida. Miongoni mwa michezo hiyo ni riadha maalum kwa wazee wenye umri wa kuanzia miaka 50.

Mbio hizo, zilizofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Mwenge, zimevutia mashabiki wengi baada ya wazee, wa kiume na wa kike, kutimua vumbi katika mbio za mita 100. Bingwa mtetezi kwa upande wa wanawake ameendeleza ubabe wake kwa kutetea taji alilolitwaa Mei Mosi mwaka 2024.

Baada ya kumaliza mashindano hayo, wazee hao walizungumza juu ya umuhimu wa kufanya mazoezi katika kuimarisha afya ya mwili wa binadamu.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments