FAINALI ya
kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika inafanyika leo Uwanja wa Lucas Moripe mjini
Johannesburg, Afrika Kusini kati ya wenyeji, Mamelodi Sundowns na Zamalek
ya Misri kuanzia 10:00 jioni.
Timu hizo zitarudiana Ijumaa ya Oktoba 21, mwaka
huu Zamalek wakiwa wenyeji wa Mamelodi Sundowns katika mechi ya Kombe
uwanjani mjini Cairo, Misri.
Zamalek
iliingia Fainali baada ya kuitoa Wydad Casablanca kwa jumla ya mabao 6-5, wakishinda
4-0 nyumbani Cairo na kufungwa 5-2 ugenini Casablanca.
Mamelodi
iliitoa Zesco United kwa jumla ya mabao 3-2 ikishinda 2-0 nyumbani baada ya
kufungwa 2-1 Zambia.
Mabingwa wa
Afrika msimu uliopita, TP Mazembe ya DRC mwaka huu hawakufuzu hatua ya makundi
baada ya kuangukia kwenye Kombe la Shirikisho.
Hata hivyo,
katika michuano hiyo midogo ya klabu barani, Mazembe imefanikiwa kufika fainali
ambako itamenyana na MO Bejaia ya Algeria Oktoba 29 katika kabla ya
kurudiana Novemba 6, mwaka huu.
0 Comments