MASHINDANO YA MEI MOSI YASHIKA KASI SINGIDA, TIMU ZA WANAUME ZAVUTA KAMBA KWA KISHINDO

 









SINGIDA

Mashindano ya kuelekea kilele cha Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) yameendelea kwa shamrashamra katika viwanja vya Bombadia, mjini Singida, ambapo timu mbalimbali kutoka wizara za serikali zimekutana kwenye mchezo wa kuvuta kamba.

Mashindano hayo ambayo yamejumuisha wizara na taasisi mbalimbali zikiwemo Wizara ya Utalii, Viwanda na Biashara, Ujenzi, Tanesco, Mambo ya Nje, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Ikulu na Mambo ya Ndani, yamekuwa kivutio kikubwa kwa wakazi wa Singida na washiriki wenyewe.

Kwa siku ya leo, pambano lilihusisha timu za wanaume ambapo mvutano mkali ulijitokeza kati ya timu za Utalii, Ikulu na Mambo ya Ndani. Timu hizi zilionyesha ushindani wa hali ya juu, huku wachezaji wakionesha nidhamu, uimara na mbinu mbalimbali za kuibuka kidedea. Timu ya Mambo ya Ndani ilionyesha ubabe kwa kuibwaga timu ya Ikulu katika moja ya michezo iliyokuwa na ushindani mkali na wa kusisimua.

Mchezo wa kuvuta kamba unatarajiwa kuendelea katika siku zijazo kwa kushirikisha pia timu za wanawake, ambapo kila timu inapambana si tu kwa lengo la ushindi, bali pia kuonesha mshikamano na kuhamasisha afya na ushirikiano kazini.

Mashindano haya yamepangwa kuanza kila siku saa 12:30 asubuhi, yakihamasisha mwamko wa michezo na ushiriki wa taasisi mbalimbali katika kuelekea sherehe za Mei Mosi kitaifa.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments