MHE. RC HALIMA DENDEGO: "TUTUNZE MAADILI, TUJENGE TAIFA!"

 


Mkuu wa  Mkoa Singida Halima Dendego akiongea na washiriki wa Semina hiyo kutoka mikoa ya Dodoma na Singida.






Sibgida

(picha na matukio mbalimbali)

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amefungua rasmi Mkutano wa Wakuu wa Shule za Sekondari wa Kanda ya Kati katika Ukumbi wa TIA – Singida.

Katika hotuba yake, Mhe. Dendego amesisitiza umuhimu wa maadili, uzalendo na uwajibikaji mashuleni, akihimiza walimu kuwa mstari wa mbele kupambana na changamoto kama utoroshaji, mimba za utotoni na kushuka kwa nidhamu.

 “Tukilea wanafunzi kimaadili, tunajenga viongozi wa baadaye.” – RC Dendego

Aidha, amewapongeza wakuu wa shule kwa kusimamia kwa mafanikio miradi ya elimu chini ya Serikali ya Awamu ya Sita, na kuwakumbusha kuhusu ushiriki wa walimu kwenye Maadhimisho ya Kitaifa ya Mei Mosi yatakayofanyika hapa Singida.

 Mkutano huu wa siku mbili unaleta pamoja wakuu wa shule kutoka Singida na Dodoma kujadili uongozi, TEHAMA, mazingira ya kujifunzia, na maboresho ya kitaaluma kupitia TAHOSA.









Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments