Mwanafunzo Shafiih Shaban akitoa neno la shukrani kwaniaba ya wanafunzi
SINGIDA
Katika kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha nguli wa muziki wa Reggae duniani, Robert Nesta Marley maarufu kama Bob Marley, Umoja wa Rasta wa mikoa ya Singida na Dodoma waliungana kwa pamoja kumuenzi kwa vitendo vya upendo na mazingira.
Tarehe 11
Mei ya kila mwaka huwa ni siku maalum ya kumkumbuka Bob Marley na mchango wake
kwa jamii kupitia muziki na ujumbe wa haki, upendo na amani. Mwaka huu, wafuasi
wa Rastafari walimuenzi kwa kupanda miti zaidi ya 200 katika Wilaya ya Ikungi,
mkoani Singida.
Mbali na
hilo, walitembelea Shule ya Msingi Ikungi, ambayo ni shule ya bweni kwa watoto
wenye mahitaji maalum, na kuwapatia msaada wa madaftari zaidi ya 100, kalamu,
na chakula, ikiwa ni ishara ya upendo na mshikamano wa kijamii.
Wakiwa
katika Kata ya Puma, Rasta hao waligawa miche ya miti ya aina mbalimbali,
ikiwemo ya matunda, kwa wakazi wa maeneo hayo. Pia walitoa elimu kuhusu umuhimu
wa upandaji miti na utunzaji wa mazingira, wakisisitiza kuwa mazingira bora ni
urithi wa vizazi vijavyo.
Katika Kata
ya Ikungi, walipanda miti zaidi ya 150 kwenye maeneo mbalimbali ya jamii na
shuleni. Akimwakilisha Mbunge wa Jimbo la Ikungi, Mhe. Miraji Mtaturu, ambaye
alikuwa bungeni Dodoma, Makamu Mkuu wa Shule ya Msingi Ikungi, Mwalimu Juma
Mpinda, aliwashukuru na kuwapongeza Rasta hao kwa moyo wao wa uzalendo na
kujitolea kwa ajili ya watoto na mazingira.
“Hii ni
hatua nzuri ya kuigwa. Tunawashukuru kwa moyo wenu wa upendo kwa jamii na kwa
kuthamini watoto wetu,” alisema Mwl. Mpinda.
0 Comments