MFANYABIASHARA AFARIKI KWA MOTO NYUMBANI KWAKE SINGIDA.

 



NA MWANDISHI WETU

MFANYABIASHARA mstaafu mkazi wa Singida mjini,Hamisi Ng’eni (61),amefariki dunia baada ya nyumba yake kuteketea kwa moto, ambayo hadi sasa chanzo chake hakijajulikana.

Mwenyekiti wa mtaa wa Unyakae manispaa ya Singida,Abbakari Athumani Kimu,amesema moto huo ulioanza kuonekana saa tatu usiku juni mbili mwaka huu.Uliendelea hadi ukateketeza karibu mali zote.

Akifafanua alisema “kwa kawaida marehemu baada ya kufiwa na mke wake miaka miwili iliyopita,amekuwa na utamaduni wa kulalal peke yake kwenye nyumba hiyo kubwa”,alisema na kuongezeka;

“Kutokana na utamaduni huo,majirani walikuja kutambua moto huo, baada ya nyumba karibu yote kushika moto”.

Alisema mwenye nyumba huyo ambaye ametolewa kwenye chumba chake cha kulala na mwanajeshi ambaye jina lake halijafahamika,hakuwa na miguu wale mikono.Yote imetekekea kwa moto.

Pia amesema wakati zoezi la kuzima moto  linamalizika,vyombo na mali zingine mbalimbali iliyokuwa katika vyumba vyote,ilikuwa imeteketa.

Jirani yake na marehemu  Ng’eni,Amita Ramadhani Idd,alisema akiwa wa kwanza kufika kwenye tukio hilo,aliokota simu ya Nge’ni  ikiwa imetupwa nje jirani na dirisha la mwenye mali.

Alisema kuwa Nge’ni baada ya kufiwa na mke wake, alianza kuugua mara kwa mara.

Katika hatua nyingine, alisema kwa sasa manispaa ya Singida,inatakiwa kuweka mikakati thabiti kuhakikisha inakuwa na vyombo vya zima moto ikiwemo maji ya kukidhi mahitati ya sasa, na wakati ujao.

“Kwa kweli huduma ya maji ya kuzimia moto,kwa sasa ipo duni kupindukia.Jana zimamoto ilipo fika hapa,ilikuwa na maji machache sana.Haikuchukua dakika,yalikwisha.Tukaanza kuhangaika huku na huko na sehemu nyingi zinazotumika kutunza maji hayo,hazikuwa na maji”,alisema kwa masikitiko.

Hata hivyo,Amita alitumia fursa hiyo kuishukru kampuni ya Maount Meru,kwa msaada wake wa kutoa msaada wa bure wa maji,na pia gari la kumbembea maji..

Kuhusu mazishi,mwenyekiti Kimu alitangaza kuwa yanatarajiwa kufanyika jana (03/06/2024) na ni  wapi atazikwa,itatangazwa watakapofika watoto wake Ng'eni kutoka jijni Dar-es-salaam.

Juhudi za kumsaka kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ili aweze kutoa taarifa ya tukio hilo,hazikufanikiwa.Baada ya kudaiwa kuwa mkuu huyo yupo nje ya ofisi kikazi yeye na msaidizi wake.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments