SINGIDA YAJIPANGA KWA SHEREHE ZA MEI MOSI – ENEO LA UBUNGO LAVUTIA WAGENI

 






 Singida | 04.04.2025

Maandalizi ya sherehe za Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) yamepamba moto mkoani Singida! Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, ameongoza ziara maalum katika eneo maarufu la Ubungo, linalotambulika kwa biashara ya nyama ya kuku wa kienyeji, hususan wakati wa usiku.

Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kujionea jinsi huduma zinavyoendelea, hasa kwa kuzingatia kuwa mkoa huu utaandaa sherehe za Mei Mosi kwa ngazi ya taifa. Akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali, akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhe. Godwin Gondwe, Meya wa Manispaa ya Singida, Mhe. Yagi Kiarau, pamoja na viongozi wa CCM mkoa na wilaya, walipata fursa ya kuzungumza na wafanyabiashara wa kuku wa kienyeji kuhusu maandalizi yao kwa ajili ya kupokea wageni.


Katika mazungumzo na Katibu wa Wachoma Kuku Ubungo, Almasi Mkoko, imebainika kuwa wafanyabiashara hao wamejipanga vyema kuhakikisha wageni wanaofika Singida kwa sherehe za Mei Mosi wanapata huduma bora.

Mkuu wa Mkoa, Mhe. Halima Dendego, amesema kuwa zaidi ya wageni elfu sita wanatarajiwa kuhudhuria sherehe hizo, na hivyo ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara wa chakula na malazi kuhakikisha huduma zao zinakuwa za viwango vya juu.


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Mhe. Yagi Kiarau, amethibitisha kuwa Manispaa imejipanga kuhakikisha usalama katika maeneo yote ya wageni, ikiwa ni pamoja na eneo la Ubungo.

 


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments