TAASISI ZA DINI MKOANI SINGIDA ZAPONGEZA AMANI ILIYOPO NCHINI


Shekh wa Wilaya Singida Issa Simba akiongea  na wananchi katika Iftari maalum iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya Singida.



                             

Katikaki ni katibu wa BAKWATA Mkoa wa Singida kushoto ni mkuu wa Taasisi ya Answli Yahaya Hussein na Kulia ni Mgeni rasmi Shekh wa Wilaya ya Singidi Mjini Issa Simba.


Katibu tawala Wilaya ya Singida Naima Chondo akitoa neno la shukrani kwa waumini na wageni mbalimbali waliyo fika katika Iftar na dua ya kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya Singida Dc na Katibu wa wilaya  hiyo wakiwa katika Dua ya kumuombea rais.



                      
                     Wageni mbali mbali waliyo udhulia kwenye Iftari hiyo wakipata futari.





                   Crip fupi ya maneno ya Shekh wa Wilaya ya Singida Shekh Issa Simba.

Singida

Taasisi za dini ya Kiislamu mkoani Singida zimepongeza hali ya amani iliyopo nchini, zikisema kuwa ni matokeo ya uongozi thabiti wa Rais Samia Suluhu Hassan na serikali yake.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Taasisi za Dini za Kiislamu Mkoa wa Singida, Sheikh Yahaya Hussein, wakati akitoa salamu katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Godwin Gondwe, katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Kwa upande wake, Sheikh wa Wilaya ya Singida, Sheikh Issa Simba, amesema kuwa amani iliyopo sasa ni matokeo ya uongozi bora wa Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan. Pia ameipongeza serikali ya mkoa wa Singida chini ya Mkuu wa Mkoa, Halima Dendego, kwa kuendelea kuimarisha mshikamano na maendeleo katika mkoa huo.                                

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Singida, Katibu Tawala wa Wilaya, Bi. Naima Chondo, amewataka wazazi kuwa makini na kuhakikisha watoto wao wanakuwa salama wakati wa sikukuu ya Eid.

Hafla hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Singida iliwakutanisha wafanyabiashara mbalimbali pamoja na viongozi wa chama na serikali.

 

 



Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments