MKAZI WA IRAMBA APATIKANA NA HATIA YA ULAWITI, AHUKUMIWA MAISHA JELA

 


Iramba -Singida

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Iramba imemhukumu kifungo cha maisha Barnaba Yohana Isaya (20), mkazi wa Kijiji cha Nselembwe, Kata ya Sherui, Wilaya ya Iramba, mkoani Singida, baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka minne, mkazi wa kijiji hicho.

Baada ya kutenda kosa hilo, mtuhumiwa alikamatwa na Jeshi la Polisi Februari 5, 2024, katika Kijiji cha Nselembwe na kufikishwa mahakamani Februari 12, 2025, kujibu tuhuma dhidi yake.

Akitoa hukumu hiyo Machi 6, 2025, Hakimu wa Mahakama hiyo, Mheshimiwa Simon Kayinga, alieleza kuwa baada ya Mahakama kujiridhisha bila shaka na ushahidi wa mashahidi, mshitakiwa alitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kitendo hicho cha ukatili.

Mheshimiwa Kayinga ameongeza kuwa adhabu hiyo iwe fundisho kwa yeyote mwenye tabia za ukatili kama huo.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments