MAFANIKIO YA JESHI LA POLISI SINGIDA: WATUHUMIWA WAWILI WAHUKUMIWA MIAKA 10 NA 30 JELA

Singida,

12 Machi 2025

Jeshi la Polisi mkoani Singida limeendelea na juhudi zake za kudhibiti uhalifu baada ya kuwakamata jumla ya watuhumiwa 28 kwa makosa mbalimbali ya jinai. Hatua hii ni sehemu ya mpango wa kuhakikisha usalama na utulivu kwa wakazi wa mkoa huu.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya jeshi hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP Aemon Kakwale, amesema kuwa jeshi lake limefanikiwa kusimamia sheria kwa ufanisi, ikiwa ni pamoja na operesheni kali dhidi ya makosa ya usalama barabarani.

Katika mwezi wa Februari pekee, makosa ya usalama barabarani 3,580 yalibainika, ambapo 3,577 yalihusisha madereva waliotozwa faini na kuruhusiwa kuendelea na safari baada ya kufuata taratibu za kisheria.

Kwa upande wa mafanikio ya kesi mahakamani, Kamanda Kakwale amesema kuwa jeshi hilo limefanikiwa kufikisha jumla ya kesi 30 mahakamani, ambapo wahusika walihukumiwa vifungo kulingana na makosa yao.

Katika hukumu hizo, mtuhumiwa mmoja amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela kwa kosa la kujaribu kubaka, huku kesi nyingine zikiendelea kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linatoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa za uhalifu ili kusaidia kudumisha amani na utulivu katika jamii.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments