MBUNGE MARTHA GWAU AZINDUA UJENZI WA NYUMBA YA MTUMISHI WA UWT SINGIDA

 




Na Mwandishi Wetu

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Mhe. Martha Gwau, amezindua rasmi ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) mkoani Singida kwa kuchangia vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 3.3. Vifaa hivyo ni pamoja na matofali, saruji, mchanga pamoja na kugharamia mafundi wa ujenzi huo.

Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Februari. Akizungumza wakati wa makabidhiano ya msaada huo, Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Singida, Bi. Martha Kayaga, amempongeza Mhe. Gwau kwa mchango wake katika hatua ya awali ya ujenzi huo.

Aidha, ametoa wito kwa wadau wengine kushiriki katika kufanikisha mradi huo ili ukamilike kwa wakati na kuwanufaisha wanachama wa UWT mkoani Singida.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments