BILION 2.1 KUTUMIKA KWA MWAKA WA FEDHA 2O22/2023 HALMASHAURI YA ITIGI

Na Nathaniel Limu. 

 BARAZA  la madiwani halmashauri ya Itigi wilaya ya Manyoni,limepitisha kwa kauli moja mapendekezo ya mpango wa bajeti  ya metengenezo ya barabara na madaraja, zaidi ya shilingi bilioni 2.1 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Kaimu meneja TARURA wilaya ya Manyoni Injinia Yose Mushi,amesema mategenezo ya barabara na madaraja kwa  halmashauri ya Itigi,yatasimamiwa na wakala wa barabara vijijini na mjini,TARURA.

Aidha,ametaja vyanzo vya mapato  kuwa ni pamoja na  mfuko wa barabara zaidi ya shilingi 638.9,fedha za jimbo shilingi milioni 500, na tozo ya mafuta shilingi bilioni moja.

Kuhusu matengenezo,aliyataja kuwa  ni pamoja na matengenezo ya kawaida  ya urefu wa kilometa 61.96, kuimarisha sehemu korofi 5.10 na matengenezo ya muda maalumu kilometa 3.92.Na  ujenzi wa barabara kiwango cha lami,cha  kilometa moja.Pingi hicho,wanatarajia kufunguzi  barabara mpya”,alisema.

Mushi ameongeza kwamba kazi nyingine ni ujenzi wa madaraja/makarabati /drift kilometa 24.Fedha zingine zaidi ya shilingi 83 milioni zitatumika katika shughuli za usimaminizi. Kazi ya upembuzi yakinifu,shilingi milioni tano,zinatarajiwa kutumika.

Baada ya kusomwa kwa bajeti hiyo,diwani wa kata ya Itigi (CCM) Alli Minja,alisimama na kuliomba baraza hilo maalum, lipitishe bajeti hiyo bila kupinga.Kwa madai imegusa kila eneo katika halmashauri hiyo changa.

Aidha,Minja alitumia fursa hiyo kuipongeza na kuishukru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia, kwa kuiongezea halmashauri hiyo fedha za kutosha, mahitaji ya halmashauri ya Itingi katika sekta zote ikiwemo ya sekta ya barabara.

“Naiomba serikali yetu sikivu,iendelee kuongeza fedha  ili barabara nyingi iweze kuboreshwa zaidi.TARURA nayo naiomba itoe kipaumbele barabara za pembezoni,kwa kuzifanyia uboreshaji ili wakulima waweze kusafirisha mazao yao, bila usumbufu wa aina ye yote”,amesema diwani Minja.

Naye mbunge wa jimbo la Manyoni magharibi,Yahaya Omary Massare,alisema ameiunga mkono bajeti hiyo, akidai  imegusa  kila eneo katika barabara za jimbo hilo.

“Binafsi nitumie muda huu kuwapongeza watendaji wa TARURA.Kwanza kwa usikivu  na uwajibikaji wao.Injinia Ogati,hongera sana.Kwa kipindi cha  awamu yangu ya ubunge,umekuwa mshauri wangu mzuri mno, wakati wote na hata usiku”,amesema mbunge huyo.

Naye mwenyekiti wa CCM halmashauri ya Itigi,Jumanne Ismael,ameutaka uongozi wa halmashauri hiyo kuongeza zaidi vyanzo vya ndani vya mapato,ili iweze kuondokana na utegemezi.

“Kwa ujumla halmashauri yetu ya Itigi,imefanya juhudi kubwa katika kutekeleza ahadi zilizopo kwenye ilani ya uchanguzi.Kwa njia hii,mtakuwa mmetupunguzia mno, uwezekano wa  sisi kuja kupingwa maswali umiza,katika uchaguzi mkuu ujao”,alisema.

Akiijengea nguvu hoja yake,alisema halmashauri imefika wakati ianze kuona aibu kila mwaka kutangaza kuwa wameletea kiasi fulani na serikali au wadau wengine.Waongeze bidii kubuni na kusimamia vizuri makusanyo yao, ya ndani.

 Eng.Yose Mushi,akitoa nasaha zake muda mfupi kabla ya kusomwa kwa bajeti ya 2022/2023 mbele ya kikao maalum cha madiwani wa halmashauri ya Itigi,ili kuipitisha.Bajeti hiyo ilipita bila ya kupingwa.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments