POLISI WAMSHIKIRIA MGAMBO KWA KUSEMA UONGO



Jeshi la polisi mkoa wa Singida, linamshikilia askari mgambo mwajiriwa wa hospital ya mkoa, Emmanuel Daghau kwa tuhuma ya kutoa taarifa za uongo juu ya maiti kufufuka ikiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya hiyo.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Singida, SSP Mayala Towo amesema tukio hilo limetokea septemba 30 mwaka huu, majira ya alasiri katika hospitali ya mkoa ambapo septemba 29 mwaka huu  Rahel Erasto (28),alifikishwa katika hospitali hiyo ya mkoa,kwa ajili ya kupata huduma ya kujifungua salama.
Aidha kamanda amesema kutokana na sababu za kitabibu Rahel, alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida na hivyo ikalazimika kufanyiwa upasuaji ambapo mtoto wa kiume alitolewa akiwa hai Lakini mama kwa bahati mbaya alifariki dunia usiku wa saa saba septemba 30, 2016
Amesema kuwa baada ya Rahel kufariki dunia, mwili wake ulipelekwa Chumba cha kuhifadhi maiti ambapo kesho yake,  ndugu walijikusanya eneo hilo wakijadiliana namna ya kuuchukua mwili kwa ajili ya mazishi Ndipo
 alijitokeza mlinzi Daghau na kuwaeleza kuwa ndugu yao huyo, alifariki kutokana na uzembe kwani akiwa kwenye doria za kawaida, alisikia marehemu akipiga chafya na aliposongelea dirishani, alimwona akiwa amefufuka.
Hata hivyo Kaimu mganga mkuu wa mkoa, Dk.Ramadhani Kabala amekiri kuwepo kwa taarifa hizo na kudai kwa sasa mwili wa marehemu unaendelea kufanyiwa uchunguzi ili kutambua kama kweli Rahel alifufuka na kupiga chafya akiwa ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti.

 Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Singida, mhandisi Mathew Mtigumwe amesema amepokea taarifa hiyo na kwamba zipo timu mbili zinaendelea na kuchunguzi ili ukweli uweze kubainika.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments