MKOA WA SINGIDA UMEBAINI KUWA NA KIWANGO KIDOGO CHA UDUMAVU

Mkoa wa Singida umebainika kuwa na kiwango kidogo zaidi cha udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, unaosababishwa na utapiamlo ikilinganishwa na kiwango hicho kitaifa.
Utafiti uliofanywa mwaka jana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto kuhusu suala la afya ya mama na mtoto unaonesha kuwa wakati kiwango cha kitaifa kwa utapiamlo ni asilimia 34, katika mkoa wa Singida ni asilimia 29.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dk Angelina Lutambi amesema hayo hivi karibuni katika hafla ya ufunguzi wa mkutano wa wadau wa Ushawishi wa Lishe ulioandaliwa na Asasi ya Mtandao wa Kiraia (Ngonedo) ya mkoani Dodoma.

Hata hivyo, Dk Lutambi amesema kiwango hicho si cha kujivunia kwa kuwa udumavu ni moja ya tatizo kubwa la lishe nchini, huathiri nguvu kazi na huchangia kwa kiasi kikubwa kuathiri uchumi wa kaya na jamii kwa ujumla.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments