HALMASHAURI WALAUMIWA KWA KUKWAMISHA UTATUZI WA CHANGAMOTO – MEYA SINGIDA





SINGIDA

Meya wa Manispaa ya Singida, Mhe. Yagi Kiaratu, amesema kuwa changamoto nyingi zinazoikabili manispaa hiyo zinasababishwa na uzembe na mapungufu ya baadhi ya watendaji wa Halmashauri.

Akizungumza katika kikao cha robo ya tatu kilichofanyika katika ukumbi wa VETA, mjini Singida, Mhe. Kiaratu alimhimiza Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha anashughulikia kero za wananchi kwa wakati, ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima.

"Tunataka kuona hatua za haraka zinachukuliwa kila mara panapojitokeza changamoto katika maeneo yetu. Wananchi wanahitaji huduma bora na majibu ya haraka," alisema Mhe. Kiaratu.

Aidha, Mhe. Kiaratu ametoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika vikao na shughuli za maendeleo ili kutoa maoni na mchango wao katika kuboresha huduma za jamii.

Kwa upande wao, Naibu Meya wa Manispaa ya Singida, Mhe. Mbua Chima, na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Singida Mjini, Bi. Luciya Mwiru, wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Manispaa hiyo.

"Rais wetu ameendelea kutujali kwa kutuletea fedha za miradi ya afya, elimu na miundombinu. Tunapaswa kuzitumia vizuri kwa manufaa ya wananchi," walisema wajumbe hao.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments