ZARI APATAMCHUMBA KENYA


 Miezi minne baada ya ulimwengu kubaini kuhusu kuwachana kwa nyota wa muziki wa bongo Diamond Platinumz na mpenziwe Zari Hassan, msanii wa muziki wa Injili nchini Kenya Alex Apoko ,maarufu Ringtone ameonyesha hamu ya kumchumbia mama huyo wa watoto watano.
Ringtone anayejulikana kwa wimbo wake 'Tenda Wema' aliyeimba na msanii wa Tanzania Christine Shusho anasema kuwa yeye ndio suluhu kwa matatizo ya kimapenzi ambayo yamekuwa yakimzonga mfanyibiashara huyo wa Uganda.
Msanii huyo sasa amemtaka mfanyibiashara huyo kutokubali kumrudia Diamond Platinumz na badala yake kukubali uchumba wake kwa lengo la kumtumikia Mungu.
''Diamond aniwachie Zari, Zari ni wangu wa Moyoni, atuwache tumtumikie Mungu'', alisema Ringtone alipotembelea afisi mpya za BBC jijini Nairobi.
Msanii huyo anasema kwamba aliota ndoto siku ambayo wawili hao waliachana ambapo anadai kumuona Zari.

Alipoulizwa kwa nini unamtaka Zari, Ringtone alikua mwepesi wa kujibu akisema kuwa ni mwanamke mrembo na mpenda biashara.
Anasema kwamba kwa kuwa amepiga hatua katika safu ya muziki anadhani kwamba Zari atamsaidia pakubwa kuendeleza biashara zake iwapo watafunga ndoa.
Vilevile amesema kuwa mfanyibiashara huyo wa Uganda ambaye kwa sasa amekita kambi nchini Afrika Kusini hafai kuumizwa na kuvunjwa moyo mara kwa mara.
Aidha amedai kwamba yuko tayari kuwakubali wanawe mfanyibiashara huyo akisema watu kutoka familia yake wanapenda watoto na kwamba nyumba yake yenye vyumba kumi ina nafasi kubwa ya kumkaribisha Zari na wanawe.
Matamshi ya mwanamuziki huyo yanajiri wiki chache baada ya Zari kuzuru nchini Kenya kwa hafla ya kampeni ya kukabiliana na ugonjwa wa saratani.
Wakati wa Ziara hiyo Ringtone alitaka kumchumbia Zari kupitia gari jipya aina ya Range Rover lakini raia huyo wa Uganda alinukuliwa na vyonbo vya habari akilikataa na kusema kuwa alikuwa amenunua gari kama hilo wiki moja iliopita.
''Kwa kweli gari nililomnunulia bado lipo na sijaamua nitalifanyia nini, mimi najua Zari ananipenda lakini ni nyinyi wanahabari ambao munampatia shinikizo kubwa. Najua kila akiamka ananitazama katika akunti yangu ya Instagram'', alisema nyota huyo wa muziki wa Gospel.
Akihojiwa na baadhi ya vyomnbo vya habari nchini Kenya Zari alikana kuwahi kuwasiliana na msanii huyo akiongezea kwamba hana haja naye na kwamba anataka kutumia wakati wake mwingi kuendeleza biashara zake na kuwaangalia wanawe.

Zari na Diamond waliwachana siku ya wapendwanao ya Valentine mwaka huu baada ya kudai kwamba nyota huyo wa muziki wa bongo amekuwa akimdhalilisha kupitia uhusiano na wanawake wengine.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments