VITUKO VYA KOMBE LA DUNIA URUSI 2018


Paka mmoja maarufu ambaye anadaiwa kuwa na uwezo wa kipekee wa kutabiri ametabiri mshindi wa mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia nchini Urusi.
Kwa mujibu wa paka huyo aliyepewa jina Achilles, Urusi ndio watakaoshinda mechi hiyo.

Achilles, paka wa rangi nyeupe ambaye ni kiziwi, hubashiri mshindi kwa kuchagua katika ya bakuli mbili ambazo zimewekwa bendera za mataifa yanayocheza.
Paka huyo ni miongoni mwa paka wanaofugwa kukabiliana na panya katika makumbusho ya Hermitage mjini St Petersburg, ingawa sasa ana majukumu hayo mapya.
Anadaiwa kubashiri kwa ufasaha mshindi wa Kombe la Mashirikisho mwaka 2017.

Paka huyo alitoa utabiri wake wa sasa Jumatano.

"Achilles yuko tayari kutumiwa kwa umma na huwa hana wasiwasi kuwa eneo lenye watu wengi," anasema daktari wa mifugo Anna Kondratyeva, ambaye humtunza.

Hata hivyo, ubashiri wake haukutimia kwani Urusi ndio waliotunukiwa hadhi hiyo.
Paul alifariki Oktoba mwaka 2010 kifo cha kawaida kulingana na hifadhi ya Oberhausen nchini Ujerumani.
Watabiri wengine
Wanyama wengine wametambulishwa kwa umma wakiaminika kuwa na uwezo wa kumrithi pweza Paul, akiwemo nungubandia, yaani guinea pig, kwa Madame Shiva kutoka Uswizi mwaka 2014.
Kulikuwa pia na samaki kwa jina Piranha Pele kutoka Uingereza.

Lakini hakuna aliyeufikia umaarufu wa Paul the Octopus.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments