MCHOMA NYAMA SINGIDA ANUSURIKA KIFO



Na Thomas Kiani
Singida

MFANYABIASHARA wa nyama choma minadani mkazi wa kijiji cha Musimi Kata ya Sepuka Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida Saidi Jumanne Mdadau(Nkimbu) (25) mwishoni mwa wiki iliyopita amenusirika kufa baada ya kutangwa njiani usiku na kupigwa na watu wasiofahamika akitoka mnadani na kumnyang’anya pesa zote na radio alionunua akaburuzwa mtoni na kuachwa hana fahamu.

Akizungumza na mwandishi jana nyumbani kwa Saidi Mtoto wake anaeitwa Ramadhani amesema siku hiyo Baba yake aliuza alizeti akanunue radio mnadani akaendelea na kazi zake lakini hakurudi nyumbani hadi asubuhi  tuliposikia ameokotwa mtoni  akiwa hoi hajitambui.

Ramadhani amesema  baba yake alitangwa njiani saa 4: 00 usiku wakati wa kurudi nyumbani akapigwa na kitu kigumu shingoni, kichwani, mgomgoni na shavuni na watu wasiofahamika akakosa fahamu pia akanyang’anywa pesa zote za mauzo na radio aliokuwa nayo akaburuzwa mita karibu 30 hadi kwenye korongo la mto huku akitoka damu akaachwa hadi asubuhi alipoonwa na wapiti njia.

Akieleza juu ya hali ya majeruhi Saidi Dada yake mkubwa Tatu Jumanne Mdandau amesema kaka yake alikuwa mtu wa kufa alipigwa akakosa fahamu, akawa hoi akaburuzwa hadi mtoni na amelala alikotupiwa baridi yote ilimuishia akiwa hapo korongoni hadi asubuhi akapelekwa Hospitali ya Mkoa wa Singida akiwa hajitambui kichwa chote kilivimba kwa majeraha lakimi Mungu amempa uzima.

Tatu ameendelea kusema hapo mapokezi Hospitali ya mkoa wa Singida walisema mmemleta wa nini huyu mtu wakati ameshakufa lakini mapigo ya moyo wake yalikuwa bado yapo, akalazwa wodi namba tatu akawekewa dripu 12 akalishwa kwa mpira japokuwa sasa amerudishwa nyumbani lakini hali yake bado tete.

Alisema
Aidha katika  tukio hilo Mwenyekiti wa kitongoji cha Italala mashariki Athumani Majuda amesema alipigiwa simu saa 1:30 asubuhi kwamba Saidi (Nkimbu) ameokotwa mtoni akiwa hoi hajitambui kichwa chote kimepigwa hawezi kusema,hawezi kuinuka na hana fahamu na alipofika alimkuta anamajeraha kichwa chote na hajifahamu.

Majuda amesema walimchukua kwa pikipiki  hadi polisi kupata hati ya matibabu wakampeleka kituo cha afya Sepuka nao wakampeleka kwa gari Hospitali ya mkoa wa Singida kutibiwa akiwa hana fahamu na ameelezwa baada ya siku nne akapata ufahamu lakini hadi sasa  hali yake sio nzuri japokuwa ameruhusiwa kurudi nyumbani.

Naye Diwani wa Kata ya Sepuka Yusufu Missanga juzi aliitisha mkutano wa hadhara kijiji cha Musimi kuzungumzia jambo hilo na yale mengine yaliyojitokeza ilibidi wanakijiji wapige kura za siri kuwataja wahalifu na akawaagiza polisi kuwakamata wote watakaotajwa ili wachunguzwe na kuhojiwa na amewataka polisi kusimamia vizuri majukumu yao kuhakikisha wanalinda mali za watu na raia zake.



Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments