NDAYIRAGIJE KUCHUKUA MIKOBA YA PLUJIM JIJI ARUSHA



TIMU ya Singida United imemthibitisha kuwa Mrundi Etienne Nayiragijje kuwa kocha wake mpya, akichukua nafasi ya Mholanzi, Hans van der Pluijm anayeondoka. 
Pluijm anaondoka Singida United baada ya msimu mmoja, akiongea na Katemanablog katibu mkuu wa Singida united Abdulhaman Sima amema kuwa Coach Ndayiragiji amekwishawasili mkoni Singida mapema kabla ya mchezo wa VPL dhidi ya  Simba na alikuwepo jukwaani akitazama mchezo huo ambapo Singida United ilipoteza kwa 1-0 katika wanjawake wa Namfua.

Sima amesema kuwa Mholanzi Hans van pluijm aliuomba uongozi wa Singida united kumuita mapema mrithi wake Mrudi Ndayiragiji ili amkabithi mikoba yake mapema baada ya mchezo wa fainali ya Azam Sports Federatin Cup (ASFC) utakao chezwa jijini Arusha na baada ya mchezo huo timu itaelekea jijini Nairobi katika michezo ya Super spots.

Ndayiragijje ambaye amekwishaachana na Mbao FC aliyoiongoza kwa misimu miwili akitokea kwao Burundi.
Msimu uliopita, Ndayiragijje pamoja na kunusurika kuishusha Mbao FC, lakini aliiwezesha kufika fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) ambako ilifungwa na Simba SC 2-1 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Na msimu huu, Ndayiragijje aliingia kwenye mtafaruku na uongozi wa klabu hiyo ya Mwanza baada ya mzunguko wa kwanza tu wa Ligi Kuu na kuondoka, nafasi yake ikichukuliwa na mchezaji wa zamani wa Pamba SC, Fulgence Novatus.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments