KIKOSI KIPYA CHA MKWASA HIKI HAPA



Nyota wa Stars walioitwa na Mkwasa ni Makipa; Deogratius Munishi 'Dida' (Yanga SC), Said Kipao (JKT Ruvu) na Aishi Manula (Azam FC).
Mabeki; Shomari Kapombe (Azam FC), Juma Abdul, Andrew Vincent, Mwinyi Hajji (Yanga SC), Mohamed Hussein 'Tshabalala' (Simba SC), David Mwantika (Azam FC) na James Josephat (Prisons).
Viungo ni Himid Mao (Azam FC), Mohammed 'Mo' Ibrahim, 
Jonas Mkude, Muzamil Yassin, Jamal Mnyate, Shiza Kichuya (Simba SC), Simon Msuva, Juma Mahadhi (Yanga SC) na Hassan Kabunda (Mwadui FC).

Washambuliaji ni Ibrahim Hajib (Simba SC), John Bocco (Azam FC), Mbwana Samatta KRC Genk (Ubelgiji), Elius Maguli (Oman) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).

Mchezo huo ulio katika kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), utafanyika mjini Addis Ababa, baada ya maombi ya Shirikisho la Soka Ethiopia (EFF).

Hii ni faida kwa Tanzania kama itashinda mchezo huo kwa maana kina alama za nyongeza kama inatokea unaifunga timu mwenyeji.
Matokeo ya mchezo huo, ni sehemu malumu kupima viwango vya ubora na uwezo wa timu za taifa. Kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya 132 kati ya nchi 205 wanachama wa FIFA zilizopimwa ubora. Ethiopia yenyewe inashika nafasi ya 126.

Argentina inaongoza ikifuatiwa na Ubelgiji anakocheza Mbwana Samatta – nyota wa kimataifa wa Tanzania. Samatta anacheza klabu ya K.R.C Genk inayoshiriki Ligi Kuu ya Ubelgiji. Timu nyingine bora kimataifa ni Ujerumani, Colombia na Brazil.


Katika Bara la Afrika, Ivory Coast ambayo ni ya 34 kwa ubora duniani ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na Algeria, Senegal, Tunisia na Ghana.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments