Ikungi
Na
Mwadishi wetu
Askari
wawili wa jeshi la akiba (mgambo) wakazi wa Kijiji cha Musimi kata ya Sepuka
wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Ramadhani Salumu (23)na Hatibu Hemedi (25)
wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao kwa kisu na nyuda Mdulu (23)
mnadani baada ya mhalifu huyo kutakiwa kituo cha Polisi kutoa maelezo walipofanya
vurugu mnadani.
Mwenyekiti
wa Kijiji cha Musimi Omari Soa amesema Askari hao wa akiba wameshambuliwa na
Nyuda Mdulu kwa kisu mnadani tarehe 30 Julai 2024 saa 10.00 jioni walipojaribu
kutia chini ya ulinzi mtuhumiwa huyo baada ya kufanya fujo mnadani Sepuka kwa
wafanya biashara ndogondogo, wananchi na wafanya biashara katika eneo hilo waliweza
kutoa ushirikiano kwa wanausalama hao nakufanikiwa kumtia nguvuni kijana huyo.
Habari
zaidi kuhusiana na tukio hilo majeruhi walipelekwa kituo cha Afya Sepuka
kutibiwa majeraha yao imefahamika |Ramadhani Salumu alichomwa kisu mkononi na mgongoni
na kushonwa nyuzi sita na Habibu Hemedi
alichomwa kisu kwenye goti , ameshonwa nyuzi sita na wanaendelea na
matibabu na hali zao zinaendelea vizuri na mhalifu ameshikiliwa na Polisi
Ikungi na baadae atafikishwa mahakamani.
Wananchi
wa Kitongoji cha Musimi Magharibi anakoishi mtuhumiwa wamesema kijana huyo
amekuwa na matukio mengi ya wizi na kugombana na watu hasa akiwa amelewa pombe
na anafanya hivyo makossa ua uhalifu kwa faida yake.
Mwenyekiti
wa Kitongoji cha Musimi Magharibi Juma Marughu amesema mwezi uliopita Nyuda
Mdulu alifanya wizi kwenye nyumba ya
mkazi wa eneo hilo hakukamatwa lakini nguo zilionekana zikifuliwa na mwenye
nguo alizifahamu akapeleka taarifa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji.
Mwenyekiti
wa Kitongoji hicho akaongozana na mwenye nguo hadi kituo cha Polisi Sepuka
kutoa taarifa, walipofika nyumbani kwa Nyuda Mdulu katika upekuzi walikuta
shuka moja wakaichukua kwa kielelezo, hata hivyo mhalifu hajakutwa alikutwa
mama yake anayeitwa Hwa Rashidi nae akachukuliwa na na Polisi hadi
kituoni.
Katika
maelezo yake kituoni sepuka Hawa Rashidi alikubali makossa ya kupatikana na
nguo ya wizi nyumbani kwake zinazodaiwa kuibiwa na mwanae huyo akaandikisha
maelezo yote na kukubaliana na mwenye nguo hizo alipe sh. 200,000/= na
alishaanza kulipa kwa mujibu wa maelezo ya Mwenyekiti wa Kitongoji Juma
Marughu.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Singida Amon Kakwale amesema makosa ya kisheria kushambuliwa askari wanaokuwa kazini,
kosa jingine kuzuia askari wasifanye kazi wanazotumwa na Serikali na Zaidi
mhalifu anajaribu kucheza na dola.
0 Comments