MAAFISA UGANI WAHIMIZWA KUTOA ELIMU BORA KWA WAKULIMA NA WAFUGAJI NCHINI


Ng"ombe wa nyama mwenye kilo 100 kutoka ASAS akiletwa kwaajiri ya gwalide maalum la wanyama wa kufugwa ni sehemu ya maonesho ya NANE NANE.



Kondoo wa kufugwa na mbuzi pia wapo kwalengola kutoa elimu ya ufugaji bora kwaajirioya kijiongezea kipatao


Dodoma

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego amewataka Maafisa Ugani nchini kuhakikisha wanatoa elimu bora kwa Wakulima na Wafugaji kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wenye tija wenye kukidhi masoko ya ndani ya kimataifa.

Wito huo ameutoa Agosti 5,2024 kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dotto Biteko wakati wa ufunguzi wa mashindo ya Paredi ya mifugo mbalimbali katika maonesho ya kimataifa ya Nane nane yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.

Aidha Mhe.Dendego amewasisitizia vijana nchini kuchangamkia fursa ya programu ya BBT yenye lengo ya kuwanyayua vijana kiuchumi kupitia kilimo

Nitoe rai kwa vijana wote nchini kuchangamkia fursa hii ili kuongeza ajira na kukuza Uchumi wa mtu mmoja mmoja na kwa taifa kwa ujumla.

Kwa upande wao, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Alexander Mnyeti na Naibu Waziri wa Kilimo David Silinde, wamewahakikishia wananchi kuwa Serikali inaendelea kuweka mipango na mikakati madhubuti ili kuhakikisha sekta hizo zinaongeza tija katika uzalishaji kama hatua ya kuwaondoa wananchi na umaskini wa kipato.

Kwa sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na zaidi ya ng’ombe Milioni 37, Mbuzi Milioni 27.6, Kondoo Milioni 9.4 na Kuku Milioni 103.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments