SHIRIKA LA AFRICA MUSLIMS AGENCY LAZINDUA KISIMA CHA MAJI SINGIDA


SHIRIKA la “Afrika Muslim Agency” (AMA) linalomiliki shirika la misaada la Direct Aid kutoka nchini Kuwait limefungua kisima cha maji cha msikiti wa Masjid  Khadri ya Ititi chenye urefu wa mita 94 kilichogharimu shirika sh. 35 milioni, katika kijiji cha Mnang’ana kitakachotumika kwa  wanakijiji 4,100 kwa kupata maji safi na salama.

Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho juzi kwa lugha ya kiarabu Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Kanda ya Afrika Sheik Mohamed Rabba ameahidi kutoa misaada  kwa wananchi wa Mkoa wa Singida ili wapate maji safi na salama ya kunywa kwa kuwachimbia visima virefu na vifupi kama moja ya imani kwa Mungu aliye muumba na mtume wake Muhammad.

Sheikh Rabba amesema katika ufunguzi huo wa kisima  kuwa mradi huo wa maji ulikuja rasmi kwa ajili ya Msikiti Mkuu wa Ititi lakini wananchi wa kijiji cha Mnang’ana wameutaka uenee kijiji chote na shirika limekubali wito huo kama moja ya malengo yake katoka nchi yake.

Sheikh Rabba amesema nchi yake Kuwait kwa kupitia Balozi wake nchini Jassem Al- Najem imejikita kuboresha maji, afya, elimu, barabara na umeme vijijini kwa wananchi wa Tanzania na sasa mkoa wa Singida.

Aidha Injinia wa shirika hilo mkoani Singida Adam Said Mussa amesema shirika lake limeamua kuweka mikakati ya nguvu kwa wananchi mkoani Singida ili waweze kwenda vizuri na kasi ya serikali kwa kuwachimbia visima vya maji vingi mahali walipo kwa ukaribu zaidi kila mita 400 kuwa na kisima cha maji salama ya kunywa.

Mussa amesema shirika lake limejikita kuchimba visima kwa kutumia mitambo ya kisasa kutoka Kuwait ili kuwawezesha wananchi kupata maji safi na salama ya kutosha kwenye maeneo yao ili waweze kupata nafasi ya kufanya mambo mengine ya kuwaletea maendeleo.

Naye kwa upande wake msimamizi wa mradi huo Singida ustaadhi Juma Rashidi Nkindwa amesema ujenzi wa mradi huo ulianza mwezi June 2017 hadi Julai ukiwa umepewa namba 30147 una mantanki mawili makubwa na umegharimu sh. 35 milioni na mafundi wa uchimbaji wamebainisha maji yalipo kwenye kisima hicho yanatosha kuwapatia maji wanakijiji mwa miaka 25.


Diwani wa Kata ya Sepuka Yusufu Missanga amewataka wanakijiji kutunza mradi huo vizuri ili utumike kwa muda mrefu kuendeza kilimo cha umwagiliaji na amewashukuru wafadhili kwa kuamua kutoa msaada huo wa maji kwa msikiti wa Masjid Khadriya na kwa  wananchi wa kijiji cha Mnang’ana na hiyo itahamasisha wananchi wenyewe kujiletea maendeleo.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

1 Comments

  1. Assalamu a'laikum warahmatullah wabarakatuh vipi Hali .

    Naitwa Albatuli, kutoka SINGIDA.

    Tunauhitajio WA kuchimbiwa kisima kwenye eneo letu lililopo ititi, Ili tuweze kufanikisha shughuli yetu ya ujenzi WA msikiti.

    Kwa mawasiliano 0785048710

    ReplyDelete