ZAIDI YA MILION 800 ZAPATIKA KATIKA HARAMBEE YA KKKT DAYOSISI YA KATI SINGIDA

 

Prof.Kitila Mkumbo Waziri wa Mipango akimwakilisha Dkt Mwigulu Nchemba kuwa Mgeni rasimi akiongea na kukabidhi michangongo yayao katika Harambee Hiyo ambapo Pref.Mkumbo alitoa zaidi ya milion 3 huku Dkt Mwigulu Nchemba akitoa Mil 5.

Mkuu wa Mko wa Singida Halima Dendego akitoa akiongea na wageni waalikwa na kukabidhi shili Mil 12 kwaniaba ya watumishi wa Serikali.

Askofu Mkuu wa Jimbo la Dayosisi ya KKKT ya Kati Singida Mjini Dkt Cyprian Hilint akitoa neno la Jimbo la kati.

Askofu Mkuu wa KKKT Tanzania Alex Malasusa akiongoza ibada Takatifu ya Harambee hiyo katika kanisa la Usharika wa Immanuel mjini Singida.

             Mfanyabiashara Tesha Vunja beia akichangia katika harambee hiyo shili laki sita.

                              Rais wa kijiji cha Nyuki Philemon Kiemi akichangia shilii laki tano.

                  
             Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii  Lazaro Nyalandu akichangia mili 105.  


                 Wabunge wa Mkoa wa Singida wakichangia zaidi ya Mil 12 kwa pamoja.




                         Burudani mbalimbali kutoka katika kwaya mbalimbali zikilindima.

Zaidi ya sh. Milioni 800 ambapo fedha taslimu ni zaidi ya milioni 700 na ahadi ni milioni 100 huku lengo lilikuwa ni kukusanya sh. Milioni 700 ili kuendeleza vituo vya elimu vya Ihanja na Kiomboi, vituo vya afya, zahanati na hospitali Singida mjini na Iambi pamoja na kuinua mfuko wa utumishi zikipatikana katika misa takatifu ya kanisa la KKKT Dayosisi ya kati usharika wa Singida Mjini.

Akiongea katika harambe hiyo Profesa kitila Mkumbo waziri wa Mipango akimuakilisha Dkt Mwigulu Nchemba aliyekuwa mgeni rasimi katiak harambee hiyo, alisema kuwa hakuna namna nyingine ya kutokomezaumasikini isipokuwa kuwekeza katika elimu.

Prof. Mkumbo amesema ili kujikomboa katika hali ya umaskini ni lazima jamii iwekeze katika elimu maana elimu inasaidia hata katika kutafakari neno la Mungu na kuliombea kanisa kuendelea kudumisha Amani, umoja na ushirikiano.

Aidha ameeleza kuwa kanisa limetoa mchango mkubwa sana katika kuchangia maendeleo nchini hasa katika sekta ya Elimu na Afya ambapo shule nyingi zimejengwa pamoja na hospitali.

Awali akimkaribisha mgeni ramsi mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amesema serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za kidini katika kuhakikisha inawahudumia wananchi.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments