MWENGE WA UHURU KUWASILI MKOANI SINGIDA -RC DENDEGO

Mkuu wa Mjoa wa Singida Halima Dendego akiongea na Wakazi wa Mkoa wa Singida  kupitia vyombo vya  Habari.

 

Na Mwandishi Wetu 

Mwenge wa  Uhuru Unatarajia kupokewa Mkoani Singida siku ya Tarehe 5/7/2024 katika Wilaya ya Manyoni Ukitokea Mkoani  Dodoma,Mapokezi hayo ya Mwenge wa Uhuru yatafanyika  Chikuyu katika shule ya Msingi Wilayani Manyoni mapema saa 12.00 asubui.

Akiongea na waandishi wa Habari Ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Singida  Halima Dendego amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika wilaya zote 5 na Halimashauri 7 kuanzia tarehe 5 na kukabidhiwa Mkoani manyara mnamo Tarehe 12.

Dendego amesema kuwa katika mkoa wa Singida Mwenge wa Uhuru Utakimbizwa kwa Umbali wa Kilometa 800.75 na kutembelea Miradi ya Maendelea 47, huku ujumbe wa Mwenge wa Mwaka huu ni “Kutunza Mazingira na Kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Taifa” sambamba na Jumbe za kudumu za Mwenge za mapambano dhidi ya Rushwa na makongamano Mbalimbali.

Aidha Dedengo ameongeza kwa kusema kuwa “Mwenge huu ni Mwenge Maalum wenye kumbukumbu ya miaka 25 ya hayati Baba wa Taifa Mwl Julias Kambarage Nyerere na Kumbukumbu ya Miaka 60 ya Mwenge wa Uhuru na Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano wetu.”

Miradi ya Maendeleo itakayo Tembelewa na kuzinduliwa na kuwekwa Mawe ya Msingi na Mwenge wa Uhuru  katika Wilaya zote 5 na Halmashauri 7 za Mkoa huu Itakuwa na dhamani ya Shilingi bili 100.12.

Akizungumzia Fedha mbalimbali zilizopatika Kwaajili ya Maandalizi ya Mwenge wa Uhuru Kwa Mwaka huu Mkuu wa Mkoa Halima Dendego amesema kuwa Wananchi wa Mkoa wa Singida wakichangia shilingi mili 287.442 huku Halmashauri zikitoa shili Mili 677.837 fedha kutoka Serikali kuu Bili 30.582 fedha kutoka kwa wahisani Bili 68.259 Wadau na Mbalimbali wa Mkoa wetu wa Singida wakitoa Vifaa na fedha taslimu vyenye dhamani ya Shili 313.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Ametoa wito kwa wanachi kujitokeza kwa wingi katika kuulaki mwenge huo utakapo fika katika maeneo yao katika Wilaya na Halmashauri zote za Mkoa huu.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments