MATUKIO YALIYO JILI KATIKA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU MKOANI SINGIDA

 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemaru Sanyamule akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego Mwenge wa Uhuru baada ya kukimbiza kwa siku nane Mkoani Dodoma ni katika Kijiji cha Cjhikuyu.





 
Hotuba za wakuu wa mikoa ya Dodoma na Singida katika viwanja vya Chikuyu Manyoni.




Sekta binafsi nichachu ya maendeleo hasa katika swala la uwekezaji katika Nyanja mbalimbali Mkoa wa Singida tutahakikisha tunaendelea kikaribisha wa wekezaji ili tuweze kufikia malengo tuliyo jiwekea.

Serikali ya awamu ya sita kupitia Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan imekuwa ikikaribisha na kutoa fursa kwa wawekezaji wa ndani na nje  ili kutengeneza ajira na kuinua uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja

Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego ameyasema alipokuwa akipokea mwenge wa uhuru Mkoa wa Singida kijiji cha Chikuyu Wilayani Manyoni.

Amesema kama Mkoa wanaendelea kuchachusha sekta binafsi katika uwekezaji ambapo imechangia sh. Bilioni 67 katika miradi ya maendeleo itakayo tembelewa, kuzinduliwa na kuwekwa mawe ya msingi na mwenge wa uhuru Mkoa wa Singida.

Dendego ameeleza kuwa miradi yote 47 imegharimu zaidi ya sh. Bilioni 100 ambayo inajumuisha sekta zote za elimu, afya, maji, mazingira, elimu, kilimo na miundo mbinu.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule wakati akikabidhi mwenge huo Mkoa wa Singida amewapongeza viongozi wanaokimbiza mwenge wa uhuru wakiongizwa na Godfrey Eliakimu kiongozi wa mbio hizo kitaifa kwa kuelezea ujumbe wa mwenge, kuhamasisha shughuli za maendeleo ,kusisitiza ufanisi na thamani ya fedha.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments