SERIKALI YAUNGA MKONO JITIHADA ZA KIMATAIFA KATIKA USAWA BI TUNU PINDA

 

            Bi Tunu Pinda akiongea na akinamama wa Mkoa wa Singida Wilayani Ikungi. 


Katibu tawala mkoa wa Singida Dkt Fatma Mganga akiongea machache kabla ya kukata keki maalum ya Harambee ya Madhimisho ya kilele cha siku ya Mwanamke Duniani.




Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa wilaya ya Singida Mjini Lucia Mwiru akiongea na waandishi wa Habari katika siku ya kilele wilayani Ikungi.. 


Serikali imeendelea kuunga mkono jitihada za kimataifa za kukuza usawa wa kijinsia ikiwa ni pamoja na kutekeleza mikakati mbalimbali ili kuwa na kizazi chenye usawa wa kijinsia.

Hayo yamesemwa na mama Tunu Pinda mke wa waziri mstaafu Mizengo Pinda alipokuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Mkoa wa Singida yaliyofanyika Wilayani Ikungi.

Tunu alisema serikali katika kuhakikisha inakuza usawa wa kijinsia imezindua kamati ya ushauri ya Kitaifa ya utekelezaji wa ahadi za nchi kuhusu kizazi chenye usawa ili kuchukua hatua za makusudi kushughulikia mifumo kandamizi kwa wananwake.

Awali akizungumza kabla ya maadhimisho hayo kuanza katibu tawala Mkoa wa Singida Fatma Mganga alisema wanawake wajitokeze katika kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwani kuna mifano ya wanawake wengi ambao waligombea nafasi za uongozi sawa na wanaume na wakashinda.

Hata hivyo mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Wilaya ya Singida Lusia Mwiru amesema Mkoa wa Singida unajivunia kuwa na viongozi wanawake ambao wameingia katika vikao vya maamuzi huku wakifanya kazi kwa weledi.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments