MTATURU AUNGA MKONO JITIHADA ZA KUPINGA UKATILI MKOANI SINGIDA.

 


Mbunge wa Ikungi Mashariki Mhe Miraji Mtaturu akiongea namna anavyoguswa na maswala ya ukatili jimboni mbele ya mgeni rasimi Bi Tunu Pinda.



Mhe Mtaturu akimkabidhi mgeni rasimi Bi Tunu Pinda Piki piki (2) kwaajiri ya kusaidia jitihada za kupinga ukatili wilayani Ikungi.


Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu ametoa pikipiki mbili kwa lengo la kusaidia jitihada za kupambana na ukatili wa kijinsia vinavyofanyika katika jamii.

Akikabidhi pikipiki hizo wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Mkoa wa Singida yaliyofanyika Wilayani Ikungi Mtaturu amesema pikipiki moja itatumiwa na dawati la polisi Wilaya ya Ikungi na nyingine itatumiwa na ofisi ya ustawi wa jamii.

Ameongeza kuwa hivi karibuni atakabidhi pikipiki nyi ngine ya tatu kwa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania SMAUJATA wilaya ya Ikungi ili kuwaongezea nguvu katika kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto.

Hata hivyo Mtaturu amesema si jambo zuri kwa baadhi ya wananchi kutoa lugha ambazo sio nzuri kwa viongozi wa serikali.

Naye mbunge wa viti maalum kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Nusrat Hanje amesema ni jambo jema kuipongeza serikali kwa kazi inazozifanya kwani sio rahisi kutatua changamoto zote kwa wakati mmoja.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments