WAKAZI WA IKUNGI MAGHARIBI WALALAMA NA UBOVU WA BARABARA YAO.

 


Na mwandishi wetu.

WANANCHI wanaotumia barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka  na Kaselya Wilaya ya Ikungi na Iramba Mkoa Singida wanalalamika barabara yao imeharibika na mvua na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa na wahusika waliokabidhiwa barabara hiyo mwezi Oktoba 2023 na Serikali sasa wanaiomba wakala wa barabara Mkoani Singida (TAN ROADS) kuitegeneza barabara hiyo.

Barabara kuu Singida hadi Ndago na Kizaga kupitia Sepuka km 77.6 ambayo kampuni ya Henan Higway ilikabidhiwa na serikali iwekewe lami sasa barabara hiyo kilometer 25 imeharika vibaya baada ya mvua kunyesha kuanzia mwezi Nov 2023 hadi Mwezi huu march 2024 kuna mashimo marefu katikati ya barabara ,mahandaki,mifereji katikati ya barabara na pembeni mwa barabara kuna makorongo mapana magari hayawezi kupita wala kupishana hivyo magari ya abiria hutumia muda Zaidi ya masaa matatu  kutoka Singida hadi Sepuka na Kaselya.

Madereva  na abiria wanaoitumia barabara hiyo hawaoni sababu ya barabara hiyo kuwa kuwa mbovu muda mrefu kiasi kile bila ya matengenezo hivyo wameomba TAN ROAD iingilie kati kunusuru hasara wanaoipata kutokana na ubovu wa barabara hivyo wamesema barabara hiyo sasa inaharibu magari yao.

Uongozi wa TAN ROAD Mkoani Singida na wale wa TARURA Ikungi wanakiri barabara hiyo kwa sasa ni mbovu kabisa hata hivyoMeneja TAN ROAD Mkoani Singida Mhandisi Massama Massama hakuweza kupatikana kuelezea marekebisho yake lakini taarifa anazo.

Barabara hii ya Singida hadi Sepuka km 17 inangojewa sana wananchi wa Wilaya za Singida Mjini na Ikungi kusafirisha abiria na mizingo  yao na mazao ya kilimo,mifugo na smaki kwenda kwenye masoko ndani ya Mkoa na Nje kwa sababu inapita kwenye maeneo yenye mikakati ya kiuchumi.

Kuanzia barabara ya Mwaru hadi Kaugeri inayoungana na barabara ku ya Singida hadi Sepuka mwezi Aprili magari makubwa ba madogo yatapita vijijini kuchukua mpunga,mchele,mahindialzeti,karanga,mbogamboga na samaki kupeleka kwenye masoko makubwa ndani ya Mkoa nan nje kwa mauzo sasa ni muhimu itingenezwe ili kurahisisha kusafirisha mazao hayo kutoka kwa wakulima na wavuvi.

Wavuvi walioko Kaugeri,Mwakanja,Magungumko na mduguyu na wale waliopo maeneo yenye samaki vijiji vya kata ya Mwaru wanaitegfemea barabara hiyo kusafirisha bidhaa za samaki kwenda mikoani barabara ikiwa mbovu namna hii watashindwa kwenda na kasi anayoitaka Rais Samia ni vema sasa itegenezwe.

Diwani wa kata ya Mwaru Idd Mkangale amasema barabara ya Singida hadi Sepuka na ile ya Sepuka hadi Kaugeri kupitia Mwaru mwaka hu itaingizia mapato makubwa Halmashauri na mapato ya kata yake kuingiza Wilaya ya Ikungi ni maratatu kuliko mapato ya mwaka uliopita kwa sababu mpunga na samaki ni wengi.

Diwani Makangale amesema wafanyabiashara wa samaki,mpunga na mchele watakuwa wengi kutoka mikoani hivyo mzunguko wa pesa katika kata yake utakuwa mkubwa licha ya kuwepo kwa mazao mengime ya kilimo na mifugo sasa ni vema baraba zitengenezwe.

 

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments