TUTASHIRIKIANA KULETA MAENDELEO YA MKOA WETU WA SINGIDA RC DENDEGO


Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Omary Dendego baada ya kuwasili mkoani Singida na kupokewa na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba hatimae rasimi amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba na kupata fulsa ya kuongea na viongozi mbalimbali wa mkoa huu wakiwemo wakuu wa wilaya,wenyeviti wa Halmashari na kamati za ulinzi na usalama.




Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba amkabidhi Ofisi mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa.

        
                Picha ya pamoja na wakurugenzi wa Halmashauri 7 wa mkoa wa Singida.

                   
                     picha na Wenyeviti wa Halmashauri 7 za mkoa Singida

                   
                                   picha na wakuu wa wilaya za mkoa Singida.

                       
                               Picha na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Singida.
 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego ameahidi kushirikiana na viongozi wengine na wananchi wa Mkoa huo kuleta zaidi maendeleo kwa jamii na Taifa na kufanyia kazi changamoto za wananchi.

 Ameyasema hayo wakati wa makabidhiano ya ofisi na mkuu wa mkoa aliyehamishwa kwenda mkoa wa Iringa kutoka Singida Peter Serukamba.

Dendego ambaye amehamishiwa Mkoani Singida akitokea Mkoa wa Iringa amesema anamshuruku Rais Samia kwa kuendelea kumwamini na kuahidi kuwa ataendelea kufanya kazi kulitumikia Taifa na kuongeza huwa watumishi wa Singida wajipange kutumia maarifa katika utendaji ili kupata majibu ya changamoto za wananchi.

 Hata hivyo kwa upande wake aliyekuwa mkuu wa Mkoa Singida Serukamba ambaye sasa ni mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema Mkoa wa Singida uko chini kiuchumi ukilinganishwa na Mkoa waIringa hivyo amejipanga kwenda kuendelea kufanya kazi kwa weledi ili Iringa iendelee kuwa juu zaidi kiuchumi. 

Serukamba amesema Mkuu wa mkoa wa sasa wa Singida Dendego ni mchapakazi na kupitia uzoefu wake katika uongozi ataleta maendeleo makubwa kwa Mkoa wa Singida.

Halima dendego amechukua nafasi ya Peter Serukamba aliyehamishwa kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa.                      


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments