MAAFISA MICHEZO MKOA SINGIDA SIMAMIENI MAENEO YA MICHEZO -RC SERUKAMBA.


Mkuu wa Mkoa Singida Peter Serukamba akiongea na maafisa michezo wa wilaya zote katika Shule ya Msingi Ukombozi mjini Singida.


Mwenyekiti wa chama cha mpira mkoa wa Singida Hamisi Kitila akitoa taarifa fupi ya mradi wa Football for School unaotaria kuanza hivi karibuni.





Mkuu wa Mkoa akitazama mipira maarum kwaajiri ya mashuleni mipira hiyo imetolewa na rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF. Wallec Karia.

 Mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba amewaagiza maafisa michezo wote kutoka  wilaya zote mkoani Singida kuhakikisha wanarudisha na kutenga maeneo ya michezo  mashuleni.

Kauli hiyo ameitoa mjini Singida katika zoezi la ugawaji wa mipira ya soka mashuleni  program inayoratibiwa na Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF..

Serukamaba amesema kuwa mipira hiyo iliyoletwa na TFF ikawechachu ya maendeleo ya michezo katika kila Wilaya Mkoani hapa.

Awali akiongea kwa niaba ya rais wa TFF Wallec Karia Mwenyekiti wa chama cha Soka Mkoa wa Singida SIREFA Hamisi Kitila amesema kuwa mkoa wa Singida umepokea jumla ya mipira 1000 kwaajili ya Mradi wa FOOTBALL FOR SCHOOLS Mradi unaotekelezwa na Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments