KUKAIMU NAFASI YOYOTE SERIKALINI MWISHO NI MIEZI SITA TU



Singida
Imeelezwa kuwa serikali baada ya kugundua kuwepo kwa uozo kwa watumishi mbalimbali wanaokaimishwa nafasi mbalimbali waliamua kuja na waraka unaoelekeza kikomo cha mtumishi kukaimu katika nafasi husika.

Kauli hiyo imetolewa na naibu waziri ofisi ya rais utumishi wa umma na utawala bora Dkt Merry Mwajerwa wakati akiongea na watumishi wa halimashauri ya manispaa ya Singida.
Amesema suala la kukaimu ndiko kunauozo mkubwa kutokana na watendaji hao kutokuwajibika kwa ufanisi pamoja na watumishi hao kukaimu kwa muda mrefu.
Naibu waziri huyo amewataka watumishi wote wa halmashauri hususani mkurugenzi na wakuu wa idara kufanya kazi kwa ushirikiano ikiwanipamoja na kupokea ushauri wa kitaalamu unao tolewa.
Katika hautua nyingine amesisitiza sauala la mafunzo katika kazi ilikuwaongezea ujuzi watumishi hao.
Ziara hiyo ya naibu wazairi mkoani Singida mbali na kukutana na kutatau kero mbalimbali za watumishi katika halmashauri za mkoa wa Singida pia anapitia 
kuangalia utekelezaji wa mpago wa kunusuru kaya Masikini TASAFU.


Naibu waziri ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Dkt Mary Mwanjelwa akiongea na watumishi wa Manispaa ya Singida katika ukumbi wa Rc Mission mjini Singida,pembeni ni mkuu wa mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi.



Wakuu wa Idara na watumishi mbalimbali wakimsikiliza Naibu waziri ukumbini hapo.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments