MTU NA MKEWE WASOMEWA MASHITAKA 50 MAHAKAMA YA WILAYA SINGIDA



Na Jenesta Zedekia
Mahakama ya  wilaya ya Singida imewasomea mashitaka  Bw.Iman Abdul  (44)na Bi.Vaileth Mangoi(34) wakikabiliwa na makosa 50 ikiwemo kula njama ya kutenda kosa na wizi wakiwa watumishi wa umma.

Akisoma  mashitaka hayo mbele ya hakimu wa mahakama hiyo wakili wa serikali Bi.Petrida Muta amesema kuwa tukio hili lilitendeka kuanzia November,2013 hadi March 2014 ambapo mishahara ya watumishi 15 wakiwemo watoro,wastaafu na waliosimamishwa kazi.

Aidha Bi.Muta amesema mishahara hiyo  ilikuwa ikiingizwa kwenye Akaunti ya Iman ambaye ni mshitakiwa namba moja kupitia Akaunti yake  namba 50802503513 NMB tawi la Singida.

Amesema kwamba katika kutenda kosa la kula njama na wizi akiwa ni mtumishi wa umma ni kinyume cha sheria kifungu cha 384 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Hadi hivi sasa kwa upande wa mashaidi wamefika watu 14 ambapo wamebakia mashaidi 5 ili kesi hiyo kukamilika kwa upande huo.
Jumla ya shilingi million ishirini na tano laki saba na kumi na tatu elfu,mia sita kumi na moja nukta ishirini na saba ilikuwa akiingia kwenye Akaunti ya mshitakiwa Namba moja ambaye ni Iman Abdul.

Hata hivyo  hakimu wa Mahakama hiyo Bi.Joyce Minde ameahirisha kesi hiyo hadi January,27,mwaka huu itakapo kuja kwa ajili ya kusikilizwa.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments