RC DENDEGO AWAITA WAWEKEZAJI SINGIDA.

 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego akiongea katika kongamano maalum katika ukumbi wa VIP nane nane jijini Dodoma.
               Katibu tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Fatma Mganga akiongea katika kikao hicho

                  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemery Senyamule akizungumza           na 
wawekezaji,wafanyabiashara waliyo fika katika maonesho ya nane nane jijini Dodoma.

Waziri katika Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe Kitila Mkumbo akiongea jijini Dodoma katika Maonesho ya Nanene ambapo wadau na wawekezaji wa ndani na nje wapo katika maonesho hayo.

Mkurugenzi wa Kijiji cha Nyuki kutoka Singida akiongea katika kongamano lililofanyika katika ukumbi wa VIP Nanene jijini Dodoma.


 Na Mwandishi Wetu


 Mkuu wa Mkoa waSingida Mheshimiwa Halima Dendego amewakaribisha wawekezaji wakubwa na wadogo kwenda kuwekeza katika mkoa huo kwa sababu tayari imeweka mazingira mazuri kwa mtu au Kampuni kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwemo Viwanda, Kilimo, Madini na Utalii.

Akizungumza kwenye Kongamano la Uwekezaji lililojumuisha wawekezaji
mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane yanayofanyika Jijini Dodoma, Mkuu wa mkoa wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amewahakikishia wawekeza watakaowekeza kwenye mkoa wake kuwa watakuwa wamechagua mkoa sahihi wa kuwekeza kwa sababu upo kati kati ya nchi na miundombinu ya usafiri ni mizuri.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa anataka kuona mkoa ya Singida unakuwa mkoa wa kwanza nchini kwenye idadi kubwa ya wawekezaji kama hatua ya kukuza uchumi wa wananchi na wa Taifa kwa ujumla kupitia fursa za uwekezaji.

 Kwa Upandewake,Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo akizungumza wakati wa kufungua Kongamano hilo la uwekezaji, amesema kwa Serikali inaendelea kuchukua hatua stahiki katika uimarishaji wa uwekezaji hasa katika sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa sababu zinamchango mkubwa katika kuinua uchumi wa wananchi na wa Taifa kwa ujumla.

 
Profesa Mkumbo amesema kwa sasa Serikali imefanya marekebisho makubwa ya sera na sheria za uwekezaji nia ikiwa ni kuondoa vitendo vya ukiritimba ambavyo vilikuwa vinakwamisha wawekezaji wengi kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali nchini.

 
Amesema mchakato huo unaenda sambamba na upunguzaji wa utitiri wa baadhi ya Taasisi mbalimbali za umma ambazo zingine ni legevu na zimekuwa kiwango katika masuala ya uwekezaji.

Kongamano hilo limehudhuriwa pia na Waziri Mkuu Mstaafu na Balozi wa Kilimo nchini Mizengo Pinda.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments