WAJINYONGA NA KUACHA PESA MEZANI

 


Na Thomas Kiani

Ikungi

Jumatatu, 11 December, 2023

WATU  wawili wakazi wa kitongoji cha Mwasija Kijiji cha Kintandea kata ya Mtunduru Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Maliki Ramadhani (31) na Shabani Hassani (45) walikutwa wamekufa kwa kujinyonga kwa kamba siku tofauti  wiki iliyopita nyumbani kwao wanakoishi wakati wake zao hawakuwepo.

 Habari zilizotolewa juzi na mwenyekiti wa kitongoji cha Mwasiya Haji Hamis Nkurwi amesema katiaka tukio la kwanza Maliki Ramadhani alikutwa amejinyonga kwa kamba  na mama yake baada ya kutomuona  nje kwa muda mrefu jambo ambalo sio kawaida yake huku mlango wa nyumba yake ukiwa umefungwa kwa ndani akaanza kutia shaka.

Akitoa maelezo kwa viongozi wa kijiji mama yake  Maliki amesema asubuhi alikwenda Singida mjini na yeye akawafungulia kuku  katika nyumba anayoishi mwanae na baadae akaendelea na shughuli zake.

Katika maelezo yake mama Maliki alisema mtoto wake aliporudi kutoka mjini alienda kwake akafunga mlango kwa ndani akafunga kamba juu ya paa la nyumba kwenye Kenchi Sebuleni akajinyonga akafa.

 Habari zinasema mama yake baada ya kutomuona mwanae nje muda mrefu akatia shaka akaenda kujua kilichomfanya asitoke, akaita sana lakini hakuitika, akasukuma mlango akaukuta mgumu umefungwa kwa ndani akaanza kuchungulia kwenye vipenyo vya mlango akaona miguu ya mwanae imeninginia.
Mama Maliki akijua mwanae amejinyonga,akaanza kulia kwa nguvu akakimbia haraka kutoa taarifa kwa watu waliokuwepo hapo nyumbani na kwa majirani na kwa mwenyekiti wa kitongoji Haji Nkurwi na walipofika wakaangalia katika vipenyo nya mlango wakashuhudia Maliki  ameninginia haraka wakatoa taarifa kwa viongozi wa kijiji

 Watu walipoingia ndani kwa kuuvunja mlango juu ya meza Sebuleni walikuta bahasha na ndani yake  ikiwa na fedha Sh 200,000/= na hazikuwa na maelezo yoyote wakatoa taarifa hizo Polisi Sepuka wakafika na kushuhudia kifo cha Maliki fedha hizo wakampa mama yake zitumike kwa mazishi ya mwanae.

Baada ya kupata maelezo ya kutosha kutoka kwa mama yake Maliki na maelezo mengine kutoka kwa viongozi wa kijiji,Polisi hawakuona shaka juu ya tukio hilo ni maamuzi yake mwenyewe  marehemu, wakatoa ruhusa azikwe kwa taratibu za dini yake.

Katika tukio jingine kitongoji hicho hicho siku nne baadae  mkazi mmoja wa eneo hilo Shabani Hassani (45) aligunduliwa amekufa kwa kujinyonga kwa kamba na mwanae wa miaka 7 saa 4:00 asubuhi wakati akicheza ukumbini na wenzake.

 Mwenyekiti wa kitomgoji hicho Haji Nkurwi amesema mwanae alipoingia ndani ya nyumba ya baba yake akashtuka kuona baba yake ameninginia, amekufa huku kamba iko shingoni imefungwajuu  kwenye kenchi.

 Baada ya kuona tukio hilo ule mtoto akatoka mbio haraka na akatoa taarifa hizo kwa watu waliokuwepo hapo nyumbani na wao wakatoa taarifa kwa viongozi wa kijiji na polisi wa kituo cha Sepuka.

Polisi wa kituo cha Sepuka walipofika na kushuhudia kujinyonga kwa Shabani na hakuna ujumbe wowote alioacha kwa familia yake na mkewe hakuwepo kwa muda mrefu yupo kwao hapakuwepo na shaka juu ya tukio hilo Polisi akaamua azikwe.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kintandaa Saidi Duyya amethibitisha kuwepo kwa matukio yote mawili kwenye kitongoji hicho na vyanzo vyake wanahisi ni ugomvi wa ndani kwa ndani na wake zao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa hakuweza kupatikana kwa simu yake lakini taarifa anazo za watu hao  na imeelezwa ni msongo wa mawazo kisa cha kujinyomga watu hao.

Mwisho.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments