Mbunge wa vijana kupitia viti maalum Mhe Nusrat Hanje akiongea na wanamichezo kutoka kata 13 za jimbo la Singida Masharaiki katika viwanja vya sekondari ya Mungaa kata ya Makiungu.
Diwani wa kata ya Makiungu Mhe John Mathias akimshukuru Mbunge Nusrat Hanje kwa kuwakutanisha vijana kwa lengo la kuhamashisha kujitokeza kwenye uchaguzi.
Mwenyekiti wa Makiungu akitoa neno la uzinduzi wa bonanza hilo kwa mgeni rasimi .
Wito
umetolewa kwa vijana kujitokeza kujiandikisha katika Daftari la mkazi sambamba
na kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi ujao.
Kauli
hiyo imetolewa na Mbunge wa Vijana viti maalum wa bunge la jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe,Nusrat Hanje katika bonanza la Vijana lililo wakutanisha vijana
kutoka kata 13 za jimbo la Singida Mashariki Wilani Ikungi.
Hanje
amesema kuwa vijana wananafasi pia ya kuongoza katika ngazi mbalimbali nchini
ikiwemo nafasi za mwenyekiti na maeneo mengine.
Awali
akizindua Bonanza hilo lililo fanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya
Mungaa iliyopo Makiungu,Mwenyekiti wa Mtaa huo Hamisi Haji amesema kuwa michezo
ni Afya michezo ni kazi kama kazi zingine huku akimpongeza Rais wa Jamuhuri ya
Muungano kwa sapoti kubwa anayoitoa katika Michezo Nchini
Naye
Diwani wa Kata ya Makiungu Mhe.John Mathias akiongea kabla ya kumkaribisha
Mbunge amempongeza Mbunge huyo kwa kuwakutanisha vijana kwa pamoja
kupitia michezo mbalimbali iliyofanyika katika bonaza hilo.
Katika
bonanza hilo Michezo mbalimabli ilikuwepo ikiwamo Draft,kukimbia na
yai,kukimbia na Gunia,Mpira wa Pete(Netball),kufukuza kuu na mpira wa
miguu,huku timu zote kutoka kata 13 zikipatiwa vifaa mabaliombali vya
michezo zikiwamo Jezi na Mpira.
0 Comments