WANAHABARI WAPIGWA MSASA JUU YA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA -SINGIDA

 

Ofisa Mahusiano Mradi wa Bomba la Mafuta  Abbas Abraham  akitoa maelezo mafupi juu ya Mradi huo.






SINGIDA

Na Mwandishi Wetu

Waandishi wa Habari Mkoani Singida wametakiwa kuendelea na utoaji Elimu kupitia taaluma ya Habari  juu ya Miradi mbalimbali ya kimkakati inayoendelea kufanyika Nchini ukiwamo Mradi wa Bomba la Mafuta unaoendelea na Ujenzi Mkoani hapa.

Ofisa Mahusiano ya jamii wa mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga Josephat Kanyunyu amewaomba waandishi wa Habari kupitia taaluma yao kutoa taarifa zinazoeleza umuhimu wa mradi huo ili wananchi waweze kuutambua kwa kina.

Ofisa huyo ametoa rai hiyo wakati akitoa taarifa ya utekelezaji na hatua iliyofikia ya mradi huo katika semina ya waandishi wa habari Mkoa wa Singida yenye lengo la kuwajengea uwezo pamoja na kupata taarifa sahihi za mradi huo wenye kambi yake mkoani hapa.

Aidha ameeleza hatua ambazo zimefanyika mpaka sasa kwa wananchi waliopisha mradi huo ikiwa ni pamoja na fidia.

Kwa upande wake Ofisa Mawasiliano wa Mradi huo nchini Tanzania, Abbas Abraham amewaeleza Waandishi hao kuwa mradi huo umefanikiwa kukwepa athari za kimazingira na kijamii.

Amesema mradi umechukua maeneo ya wananchi takribani 9,000 kutoka katika mikoa yote ambayo mradi umepita  na wamekwisha lipwa fidia.

Hata hivyo wanahabari hao wametoa wito kwa wasimamizi wa mradi huo kuwashirikisha Waandishi wa Habari ili wawe na taarifa sahihi na kuifahamisha jamii kuhusu mradi huo wenye manufaa kwao na Taifa kwa ujumla.

Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda umepita katika Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma hadi Tanga.

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments