KASI YA KUSHUKA KWA MAADILI MANISPAA YA SINGIDA YAONGEZEKA -SHEKH SIMBA


                                      

Sheikh wa wilaya ya manispaa ya Singida,Issa Ramadhan Simba (aliyesimama) akitoa nasaha zake kwenye kilele cha maadhimisho ya Idd al Adha yaliyofanyika kwenye uwanja wa Ipembe mjini Singida jana.

 

Sheikh wa wilaya ya manispaa ya Singida,Issa Ramadhan Simba (aliyepinga magoti wa kwanza mbele) akishiriki maombi  kwenye  kilele cha maadhimisho ya Idd aL uedhhiya, yaliyofanyika kwenye uwanja wa Ipembe mjini Singida jana.

Katibu wa BAKWATA mkoa wa Singida Burhan Mlau,akitoa nasaha zake kwenye kilele cha maadhimisho ya sherehe za Iddi Al-Udhhhiya (chijo) kwenye uwanja wa Ipembe mjini Singida.

Na Mwandishi Wetu

 Kasi ya kushuka kwa maadili ya watoto wa halmashauri ya manispaa ya Singida, kunatishia halmashauri hiyo kuwa na vijana wenye maadili mabaya na  wasiokuwa na hofu ya Mungu.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa maadhimisho ya sherehe ya Idi al adha  (Chija) ya siku tatu, sheikh wa manispaa ya Singida Issa Ramadhan Simba alisema hivi sasa vijana wengi wamepotoka na kusahau maadili yaliyo mema.

“Kwa kweli tuna mmonyoko mkubwa wa maadili hasa kwa watoto wetu tunaongoza kwa maporomoko hayo  mabaya.Tujifunze kutengeneza maadili mema kwa watoto wetu,ili tuwe na kizazi chema mbele ya safari”,ameongeza.

Amewasihi  wazazi/walezi kupitia Eid hiyo kila mtu atazame au afuatilie nyenendo za watoto wake kama zinazingatia maadili mema Endepo kuna mtoto anakwenda kinyume basi arekebishwe mapema.

Pia sheikh Simba amewataka wakazi wa wilaya hiyo,kuiombea nchi ipite salama kipindi hiki cha kuelekea uchanguzi  wa serikali za mitaa.

Awali Katibu wa BAKWATA mkoa wa Singida,Sheikh Burhan Mlau,alisema dunia nzima sasa hivi inaadhimisha sherehe ya Eid al adha Hivyo waumini wanapaswa kuisherehekea kwa utulivu.

Katika hatua nyingine,Sheikh Mlau,ametumia fursa hiyo kumshukuru sana Rais Dk.Samia Suluhu Hassan,kwa uongozi wake ambao pamoja na mambo mengine mazuri,amepelekea nchi kuwa ya amani na utulivu mkubwa.

Aidha ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa manispaa ya Singida  kujitokeza kuomba nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Kwa mujibu wa  Mlau manispaa ya Singida imepata ng’ombe 7,000,mbuzi na kondoo 20,000 kutoka nchi za Misri na Uturuki.Kwa ajili ya maadhimisho ya Eid al adha kwa wakazi wa manispaa ya Singida.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments