BABU AKATWA NA SHOKA NYUMBANI KWAKE.

 


MKAZI wa Kitongoji cha Kibaya Kijiji cha Nsongambele Kata ya Ndago Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Juma Shabani (80) amekutwa amekufa asubuhi na Mkwe Tatu Selemani nyumba anayolala alipoona miti ya uzio wa zizi la ng’ombe haujaondolewa akatia shaka akaenda anakolala mume wake kujua kilichomfanya asifungue miti ya zizi la ng’ombe.

Imeelezwa, mke wake Tatu Selemani alipofika kwenye mlango wake alikutana na damu, roho ikamruka akabaini mume wake Mzee Juma amekufa, amekatwa kichwa upande wa kushoto na kitu chenye ncha kali kinachodhaniwa kuwa ni shoka.

Akitoa habari hizi kwa simu ndugu wa karibu (jina tunalo) amesema tukio hilo lililotokea mwishoni mwa mwezi uliopita usiku wakati watu wamelala na mzee Juma akiwa amelala kwenye nyumba nyingine.

Mtoa habari amesema Mzee Juma aliingiliwa usiku na watu wasiojulikana akiwa amelala kwenye nyumba yake isiyokuwa na mlango akakatwa kichwa upande wa kushoto juu ya sikio na chini ya sikio kwenye shavu hadi ndani ya ulimi kupitia meno yake, alikatwa pia kisogoni na hasa ndicho kilichomfanya ashindwe kupiga kelele.

Habari zinasema Tatu Selemani alipofika nyumbani anamolala mume wake alikuta damu, akapiga kelel kwa nguvu Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kibaya alifika akiwa na majirani zake Ramadhani Buko, akasaidia kutoa taarifa kwa viongozi wa kijiji na kata, walifika na kuhuhudia tukio hilo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsongambele Martin Manase amesema amezipata taarifa hizo za tukio hilo asubuhi kutoka kwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha kibaya Ramadhani Buko na alipofika na kuhudia tukio hilo akatoa taarifa Polisi Ndago na Wilayani Iramba.

Polisi walipofika wakafuatana na Waganga kushuhudia tukio hilo na katika uchunguzi wao walibaini mzee Juma Shabani alikufa kutokana na maumivu ya majeraha ya kukatwa kichwa na kitu chenye ncha kali kilichosimama wima kinachodhaniwa kuwa ni shoka hata hivyo sababu za kuuawa kwake hazikufahamika na waliomuua bado hawafahamiki mpaka sasa.

Habari kutoka familia yam zee huyo zinasema Mzee Juma Shabani aliingia kitongoji cha Kibaya kijiji cha Nsongambele wilayani Iramba mwaka 1962 akamiliki eneo kubwa la kilimo na mifugo anawa watoto na vijukuu na alikuwa ana mahusiano mazuri na wananchi wenzake na viongozi wa eneo hilo.

Polisi imewashikilia watu wanne akiwepo mke wake Tatu Jumanne kwa uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo, Polisi wanaendelea na uchunguzi wao ili kujua kisa cha mzee huyo kuuawa.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments