FISI WALETA KIZAAZAA KWENYE MAKAZI YA WATU (W) IKUNGI.

Na Mwandishi wetu (w) Ikungi

KUMEKUWA na kundi dogo la fisi wanao zunguka usiku kwenye makazi ya watu kitongoji cha Mrama Kijiji cha Musimi Kata ya Sepuka Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida wamekula mbuzi,kondoo na mbwa na kutishia maisha ya wakazi wa eneo hilo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mrama Athumani Kijanga amethibitisha kuwepo kwa kikundi cha fisi kwenye eneo lake wiki mbili sasa na tayari wamekula mbuzi 2 kondoo 1 na mbwa 1 lakini hakuna mtu aliye ripoti wakushambuliwa na fisi japo kuwa watu kadhaa wamekutana na fisi usiku.

Fisi hao ambao inasemekana kuonekana kwenye makazi ya watu saa 12:00 jioni na asubuhi saa 12:00 amesema kuwa wanyama hao wanatashia amani kwa wakazi wa eneo hilo hasa wakulima mashambani  kwenye mashamba ya Mtama,uwele na alzeti mkazi wa kijijini hapa Hamisi Saidi alitaka kung’atwa na fisi shabani kwake.

Habari zilizopatikana  kutoka kitongoji hicho cha Mrama zilizotolewa na mmoja wapo wa wakazi wa eneo hilo Antony Jakobo zinasema watoto wake juzi saa 12:00 jioni wali kwenda kuchota maji mbugani wakati wanarudi wakakutana na fisi akifukuzwa na kunguru wakalitupa galoni la maji wakakimbia fisi huyo akaenda kulichukua galoni hilo kwa meno yake akaishia nalo vichakani lakini baadae alikimbilia kwenye mashamba na akutokomea.

Kwa mujibu wa Antoni Jakobo fisi hao wamekula mbuzi mbili kwenye mji wa Juma Omari, wamekula Kondoo mmoja kwenye mji wa Miraji Juma na kwenye mji wa Juma Wawa wameondoka na mbwa wake na Hamisi Saidi alikutana na fisi saa 3:00 usiku wakiwa nane akakimbia akiogopa kushambuliwa na fisi hivyo ni wazi kuwa fisi waka sasa kwenye maeneo ya watu wakisaka chakula.

Afisa Mtendaji Kata ya Sepuka Abella Kibanda  katika mahojiano mafupi juu ya  kuwepo kwa wanyama hao kwenye makazi ya watu kitongoji cha Mrama amesema ni kweli fisi wapo katika eneo hilo la Mrama wahitokea kwenye hifadhi ndogo za vijiji wanadaiwa wamekula mifugo ya watu na kutishia maisha ya watu lakini ofisi yake bado haina taarifa rasmi hivyo anashidwa kuelezea vizuri.

Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA) imetoa wito kwa viongozi wote wa vijiji vilivyopo kwenye hifadhi kubwa na hifadhi ndogo za vijiji walipo wanyama hawa fisi mara tu wanapoanza kuonekana kwenye makazi ya watu kushambulia mifugo na kutishia maisha ya watu ni muhimu watoe taarifa mapema ofisi za viongozi wa Kata na Vijiji na zaidi ofisi za wanyamapori zilizokaribu ili udhibiti ufanyike kabla madhara makubwa hayajafinyika.

=MWISHO=

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments