WANAFUNZI 15 WAFAULU SEPUKA SEKONDARI -(W) IKUNGI.



Jumla ya Wanafunzi 15 kati ya wanafunzi 69 wa Shule ya Sekondari Sepuka Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida wamefaulu mitihani yao ya  kidato cha nne mwaka 2023.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa  na makamu wa Mkuu wa Shule hiyo Abubakari Amasi zinasema mwaka 2023 wanafunzi 69 walifanya mitihani ya kidato cha nne waliofaulu vizuri ni wanafunzi 15 katika viwango vya division ya kwanza hadi ya tatu.

Mwalimu Amasi anasema katika taarifa yake kuwa kiwango cha division ya nne wanafunzi 47 walichaguliwa na wanafunzi 7 wapeta division 0.

Katika taarifa yake mwalimu Amasi alibainisha kuwa katika division ya kwanza wanafunzi 2 wamefaulu, katika division ya pili waliopita ni mmoja na katika division ya 3 wanafunzi waliofaulu ni 12 hivyo division ya 4 ni 47 na mwisho division ya 0 ni 7.

Shule ya sekondari ya Sepuka ilipata namba ya usajili 797 mwaka 1998 ina walimu 16 kwa miaka miwili mfululizo 2020-2021 ufaulu ulikua mdogo na shule kuapata alama ya kiwango hali hiyo iliwafanya wazazi na wadau waanze kulalamika ufaulu ulikuwaje na kitu gani kilisababisha.

Wazazi na wadau wa elimu wamesema viwango katika shule hiyo vilichukua miaka miwili lakini sasa shule iliweka mikakati kuanzisha kambi mapema kuanzia mwezi Juni hadi Sept 2023 kwa maelezo ya uongozi wa shule ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi watakaofanya mitihani walimu na wanafunzi wakajibidisha katika masomo yao yote na matokeo yakawa mazuri.

‘‘Mwaka 2023  na mwaka huu walimu na wanafunzi watafanya bidi kuongeza ufaulu na shule inategemea kuweka kambi mapema ili wanafunzi wafaulu vizuri masomo yao.” Alisema mwalimu Amasi

Wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo wamefurahi mno kuona Watoto wao wamefaulu kuendelea na masomo shule za juu hivyo wamewataka walimu kuongeza bidi katika ufundishaji.

Walimu wa shule hiyo wamewataka wanafunzi waongeze bidi kusoma masomo yao ili matokeo yam waka huu 2024 yawe mazuri Zaidi kuliko mwaka uliopita wamewataka wapambane masomo yao kufaulu hawataki kuona shule yao inapata alama ya ziro kwa wanafunzi.

Shule ya Sekondari Sepuka yenye walimu 16 ikishirikiana na wazazi na wanafunzi wa shule hiyo jitihada zao zimeongezeka ufaulu kuliko mwaka uliopita hasa baada ya kuweka kambi miezi4.

Mwaka huu 2024 shule hiyo imepanga kuhakikisha ufaulu unaongezeka kwa wanafunzi wengi kwa sababu walimu wamepanga kuweka kambi mapema ili wanafunzi wapate muda wa kutosha na kuelewa masomo ili waje kufanya mitihani yao.

Wazazi wametoa raia kwa serikali kwamba uanzishwaji wa kambi kwa madarasa yenye mitihani ya kitaifa ni moja ya nja kuu ya kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa madarasa hayo basi serikali iridhie na iweke wazi ifahamike na itumike na wao hawana kipingamizi.

Nao wadau wa elimu wamesema shule ni viwanda vinavyozalisha bidha bora, walmu ni mashine na wanafunzi ni malighafim za viwanda na ili zizalishane bidhaa bora ni lazima serikali isimamie vizuri mazingira yake.

  

 

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments