VIJANA WAKIUME WAIOMBA JAMII KUWAKUMBUKA

 

Katibu tawala mstaafu mkazi wa wilaya ya Manyoni,Doroth Aidan Mwaluko,akitoa nasaha zake kwenye maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Manyoni mjini.

 


Baadhi ya wanafunzi kutoka shule za msingi na sekondari waliohudhuria maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Manyoni.

Baadhi ya wanafunzi kutoka shule za msingi na sekondari waliohudhuria maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Manyoni.


Picha ya pamoja wanafunzi wa shule na msingi na sekondari shule za wilaya ya Manyoni,baada ya kuhudhuria maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani.Picha na Nathaniel Limu.

VIJANA wa kiume shule za msingi na sekondari wilaya ya Manyoni mkoani Singida,wameiomba jamii isiwasahau katika kushiriki masuala mbalimbali ya kijamii,kiuchumi na kiutamaduni.

Ombi hilo limetolewa na vijana wa kiume wa sekondari ya Kilimatinde  na St.John’s  zote za wilaya ya Manyoni.Vijana 250 wa kiume na kike kutoka shule ya msingi Kilimatinde na St.John’s,walikutana pamoja kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Akizungumza kwa niaba ya vijana wa kiume,Silvester Saniani,alisema kuwa jamii ya sasa imeweka kipaombele zaidi,kwa watoto wa kike kuliko wa kiume.

Ameongeza kwamba  kuanzia ngazi ya familia,shuleni na maeneo mengine,vijana wa kike wamekuwa wakipewa vipaombe zaidi.

“Kijana wa kiume hata akichelewa kurudi nyumbani, hakuna mtu anayefuatilia.Ikitokea kwa bahati mbaya kijana wa kiume akijiunga na kundi lisilo faa,jamii  haitachukua hatua yo yote kumrejesha kwenye maisha salama.Wazazi na jamii,watamwona mwanafunzi ana acha shule,hakuna atakayejali”,amesema kwa masikitiko.

Mwanafunzi huyo ametumia fursa hiyo kuiomba  jamii kwa ujumla,iungane pamoja kuhakikisha vijana wa kiume wanapewa vipau mbele, kama inavyotokea kwa vijana wa kike.

Katika kilele cha maadhimisho hayo,wanafunzi walipata fursa kujadili mambo mbali mbali.Pia walifundiswa juu ya  chimbuko la Siku ya wanawake Duniani.Somo hilo lilitolewa na mwalimu Dorothy Aidan Mwaluko katibu tawala mkoa mstaafu.

Mwaluko amewataka wanafunzi hao wahakikishe wanasoma kwa bidii,na wazingatie yote wanayofundishwa.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wa kike,Gradness Jodocas,alitumia fursa hiyo kumshukru afisa vijana mkoa wa Singida,Frederich Joseph,kwa uamuzi wake wa kuendeleza program ya malezi na makuzi mema, kwa vijana katika mkoa wa Singida.

Amemsihi asichoke na badala yake aongeze kasi katika kusimamia malezi na makuzi kwa vijana,ili kuwa na kizazi chenye hofu ya Mungu.

Kongamano hilo lililofana,pia lilihudhuriwa na afisa michezo mkoa wa Singida,Amani Mwaipaja,afisa tawala wilaya ya Manyoni Leila Same,Viongozi wa madhehebu ya dini na walimu kutoka shule shiriki.

Hata hivyo,mkazi wa kijiji cha Ihanja wilaya ya Ikungi,Isekuu Mwantandu,amewaomba wanafunzi wa kiume wilaya ya Manyoni,wawe wavumilivu kipindi hiki ambacho jinsia ya kike inapata haki zao kwa mujibu wa sheria zilizowekwa.Hakuna upendeleo wo wote wanaoupata wanafunzi wa kike.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments