RUWASA SINGIDA DC YATEKELEZA MIRADI YA MAJI.

Eng Athumani Mkalimoto Meneja wa wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA Halmashauri ya wilaya ya Singida akitoa taarifa ya miradi mbalimbali katika kikao Baraza la Madiwani.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Singida Mhe Elia Digha akifunga kikao cha baraza la madiwani katika ukumbi wa Halmashauri hiyo uliyopo katika mjimdogo wa Ilongero.


Baada ya jumuiya ndogo ndogo kushindwa kujiendesha katika mradi wa maji vijijni ikiwamo kulipa mishahara,umeme na Wizara ya maji nchini imetoa muongozo kwa mameneja wa ruwasa  kuhakikisha wanaunganisha jumuiya zote kwa lengo la kuleta tija na kupunguza usumbufu kwa watumiaji wa maji hasa vijijini.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja Ruwasa Halmashauri ya Wilaya ya Singida  Eng Athumani Mkalimoto  wakati akitoa taarifa ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Mkalimoto amesema kuwa kwa Wilaya ya Singida mpaka sasa kuna zaidi ya jumuiya 23 hivyo basi jumuiya hizo zitaunganishwa kutoka 23 na kubaki na jumuiya 8 tu, ambapo amewata madiwadi kuunga mkono hatua hiyo kwani inalengo la kuboresha huduma ya maji.

Akijibu maswali yaliyoulizwa na madiwani hao wakitaka ufafanuzi zaidi juu ya mfumo huo mpya uliotolewa na Wizara ya maji nchini Eng Mkalimoto amesema tatizo kubwa lililo jitokeza ni baada ya ubadhirifu wa fedha uliotokana na wafanyakazi wa jumuiya hizo kushindwa kusimamia miradi hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmshauri ya Singida Mhe Elia Digha akifunga mkutano huo amewataka watendaji na watumishi wa Halmashauri kuhakikisha wanasimamia mapato ili kufikia malengo ya mapato waliyojiwekea.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments