MKURUGENZI SUMACO APONGEZA UONGOZI WA SHULE YA MISUNA, ATAKA WANAFUNZI WAJIFUNZE MAADILI

                              

Mkurugenzi wa Summaco Eng Co.Ltd Fenny Mashanjala akiongea katika maafali ya shule ya Msingi Misuna. 

   

 Mwenyekiti wa kamati ya Shulea ya Msingi Misuna akiongea na wazazi juu ya Shulea.

          

                  Mkuu wa Shule ya Msingi Misuna Karoli Urassa akitoa taarifa fupi ya shule hiyo.


SINGIDA

Waalimu na uongozi wa Shule ya Msingi Misuna iliyopo Kata ya Misuna, Manispaa ya Singida, wamepongezwa kwa mchango wao mkubwa katika malezi na elimu bora ya watoto.

Pongezi hizo zimetolewa na Mdau wa Maendeleo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Sumaco Engineering Company Ltd, Fenny Msahanjala, wakati wa sherehe ya mahafali ya Darasa la Saba shuleni hapo.

Mashanjala alisema licha ya changamoto zilizopo, bado ni muhimu kuendelea kuwafundisha wanafunzi siyo tu masomo darasani, bali pia maadili ya Kitanzania ili wawe raia wema na wenye maadili mema.

Aidha, baada ya kushuhudia igizo lililooneshwa na wahitimu likiwa na maudhui ya harusi na wapambe wao, Msahanjala alitoa angalizo kwa walimu na wazazi kuhakikisha michezo ya watoto inazingatia maadili na umri wao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule hiyo, Mwalimu Karoli Urassa, alieleza kuwa shule ya Misuna kwa sasa ina wanafunzi 1,890, lakini ina walimu 26 pekee na madarasa 18, hali inayosababisha upungufu mkubwa wa rasilimali za ufundishaji.

Aidha, aliongeza kuwa shule hiyo ina madawati 330 pekee kati ya mahitaji ya madawati 630, na pia walimu hawana vyoo vya matumizi yao. Alitoa wito kwa serikali na wadau wa elimu kushirikiana kutatua changamoto hizo.

Awali, Mwenyekiti wa Kamati ya Shule, Elimboto Majengo, alihimiza wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya wanafunzi pamoja na kushiriki katika ununuzi wa madawati ili kuimarisha ufaulu wa wanafunzi.

Sherehe hiyo ilihudhuriwa na wazazi, walimu pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo ya elimu mkoani Singida.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments