ASKARI 90 WA MGAMBO WAHITIMU MAFUNZO IRAMBA

 

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda akiongea na Askali hao baada ya Kuhitimu Mafunzo yao.





Na Mwandishi wetu 

Iramba -Singida

Askari 90 wa Jeshi la Akiba, wakiwemo wanaume 62 na wanawake 28, wamehitimu mafunzo ya zaidi ya miezi minne ya mgambo yaliyofanyika katika Kata ya Ulemo, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Akifunga mafunzo hayo Agosti 26, 2025, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Yusuph Mwenda, aliwapongeza wahitimu kwa nidhamu na kujituma kwao hadi kufanikisha kuhitimu mafunzo hayo. Aliwataka kuwa mabalozi wa amani na uzalendo katika maeneo yao.

Vilevile, DC Mwenda aliwashukuru viongozi wa Kijiji cha Kitukutu kwa ushirikiano wao uliowezesha mafunzo kufanyika kwa mafanikio makubwa. Amesisitiza kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuwapa kipaumbele vijana waliopitia mafunzo ya mgambo, ikiwemo nafasi za kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na majukumu mengine ya kitaifa na kijamii.

Kwa upande wake, Mshauri wa Mgambo Wilaya ya Iramba, SSGT Omari Jabu Kidawa, alisema jumla ya vijana 90 walijiunga na mafunzo hayo, ingawa 11 walishindwa kuhitimu kutokana na utoro.

Aliongeza kuwa masomo waliyofundishwa yamelenga kuwajengea uzalendo, nidhamu, ukakamavu na utayari wa kushiriki kikamilifu katika majukumu ya kitaifa.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments