MAANDALIZI YA BONANZA LA PASAKA SINGIDA DC GONDWE MGENI RASIMI.

 

                           Edwin Christopher Mwenyekiti wa Singida Veteran na Mratibu wa Bonanza la Pasaka. 

                         

Eva Pascal Mwenyekiti wa Singida Veteran Netball akiongea juu ya maandalizi ya Bonanza la Pasaka kwa upande wa Mpira wa Pete Netball.

Said Mustafa katibu wa Singida Veteran (SIVET) lengo la bonanza hili la Siku kuu ya Pasaka ni kujenga umoja wa timu za Veteran Mkoani Singida 



Mkuu wa wilaya ya Singida Godwin Gondwe anatarajiwa kuwa mgeni rasimi katika bonanza la kusherehekea sikukuu ya pasaka,bonanza hilo linaloratibiwa na timu ya Veteran Singida litakutanisha timumbalimbali  kutoka  Mkoani Singida na viunga vyake.

Akiongea na waandishi wa Habari Mwenyekiti  wa kamati ya maandalizi ya bonanza hilo  Edwin Christopher amesema kuwa kwa mawaka huu hawata safari  nje ya Mkoa  kama ilivyozoeleka na wameamua kufanya bonanza maalum la Pasaka na pia wamemuomba mkuu wa wilaya Godwin gondwe kuwa mgeni rasimi katika bonanza hilo.

Christopher amesema kuwa bonanza hilo litakuwa na michezo ya mpira wa miguu na mpira wa pete yani Netball likichagizwa na burudani mbalimbali na nyama choma vyakura mbalimbali na kwa wale waliofunga mwezi mtukufu watakuwa na chakura maarum baada ya mfugo kuanzia saa 1:00 jioni.

Naye katibu wa Veteran Singida (SIVET) Saidi Mustafa amesema kuwa Lengo la bonanza hilo ni kutengeneza ushirikiano baina ya timu mbalimbali za Veteran ambazo zinapatikana katika Mkoa huu wa Singida.

Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments