UPEPO MKALI WANG'OA MABATI NYUMBA 9 IKUNGI.


Picha kutoka maktaba

KIMBUNGA na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa umeng’oa mabati ya nyumba 9 na kuharibu nyumba moja ya tembe Kitongoji cha Mayuyuda Kata ya Sepuka Wilaya ya Ikungi mkoani Singida na kusababisha familia Zaidi ya 10 kukosa makazi japokuwa hakuna aliyejeruhiwa lakini hasara kubwa imejitokeza uharibifu wa mali, mashamba na nyumba zote zikiwa na thamani ya sh. 50 milioni.

Imeelezwa familia za nyumba hizo hawana makazi wanaishi kwa ndugu zao baada ya nyumba 9 kati ya 10 kuharibiwa na kimbunga hicho kikali kilichofuatana na mvua tarehe 28/1/2024 saa 12:00 jioni na kuharibu chakula kilichokuwepo ndani ya nyumba.

Akitoa katika \kitongoji cha Mayuyuda Mwenyekiti wa Kitongoji hicho Jumanne Ighembe amesema nyumba 9 paa zake zimeng’olewa na kimbunga hicho siku hiyo jioni huku nyumba ya tembe imeharibiwa vibaya ba mvua na upepo wake.

Ighmbe amewataja wanakijiji ambao nyumba zao zing’olewa bati ni pamoja na Shabani Kiseke nyumba 3, chakula gunia nne za mahindi na kuku 10 wamekufa.

Katika nyumba ya Shabani Jafari bati zimeng’olewa, baiskeli na dram moja la lita 100 na wakati huo huo nyumba ya Mzee Mussa Shabani imeng’olewa bati, baiskeli imeharibiwa na migomba imevunjwa vunjwa yote.

Kwa mujibu wa Ighembe nyumba Batuli Juma imeng’olewa na upepo magunia 2 ya mahindi yameharibika, vyombo vya ndabni havipo, nguo hakuna na dramu la  plastiki la lita 100 limesombwa na maji.

Katika mkasa huo nyumba mbili za bati za Mwanahamisi Masimba  zimeezuliwa paa na upepo mkali, nguo zimechukuliwa, mahindi gunia mbili na  uwele, vyombo na kitanda kimevunjika.

Katika taarifa yake juu ya tukio hilo Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnang’ana Paskal Mdimi amesema mashamba eka 25 za mazao mbalimbali yameharibiwa na upepo huo ulioambatana na mvua kubwa.

Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Skelita Kagaruki amesema gharama za nyumba zilizoharibiwa na kimbunga iliyoambatana na mvua Kitongoji cha Mayuyuda ni sh. 35 milioni na vyombo vilivyoharibiwa pamoja na kuku 10 ni sh. 5 milioni na mashamba ekari 25 zimeharibiwa vibaya hata hivyo tathimini yake haijajulikana.

Diwani wa Kata ya Sepuka Halima Ng’imba ametoa pole wote waliopatwa na mkasa huo tareyhe 28/1/2024 nyumba zao kung’olewa na upepo huo uliosababisha uharibifu mkubwa wa nyumba, chakula, vyombo na mashamba Zaidi y ash. 50 milioni zinahitajika  kuwasaidia waathirika katika kitongoji cha Mayuyuda Kijiji cha Mnang’ana.

Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha kila siku mkoani Singida mwaka huu 2024 zimeharibu barabara zote za Moramu ndogo na kubwa vijijini, nyumba nyingi zimeharibika na chakula yakiwemo mashamba ya mazao mchanganyiko ya chakula na biashara hata hivyo maeneo mengine watafanikiwa kupata chakula cha kutosha lakini maeneo baadhi yatakubwa na njaa kama hawatalima viazi na mihogo.


Tuandikie Maoni Yako Hapa

Post a Comment

0 Comments